HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 12, 2019

SERIKALI YA MKOA WA TABORA KUTOWAVUMILIA WALIMU WANAOZALISHA SIFURI NYINGI

Mwenyekiti wa  umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari (TAHOSA) mkoani Tabora  Penini Shani akitoa salamu za umoja huo wakati wa Mkutano wa TAHOSA Mkoa wa Tabora hivi karibuni.


 NA TIGANYA VINCENT
 
SERIKALI ya Mkoa wa Tabora imesema haitasita kuwachukulia hatua Wakuu wa Shule za Sekondari na Msingi ambao watakuwa na wanafunzi wengi waliopata Daraja la nne na Sifuri.

Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Msalika Makungu wakati wa mkutano wa umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari (TAHOSA) mkoani Tabora.

Alisema Shule zinazozalisha sifuri na Daraja la nne (division four) kwa wingi ndizo zinasababisha Mkoa wa Tabora kutoshika nafasi ya kwanza katika matokeo mbalimbali ya kumaliza elimu ya msingi na Sekondari.

“Hatutasita kumchukulia hatua wale wanaotuvutavuta shati tuzifanye vizuri na hivyo kuwa na watoto waliopata sifuri na Daraja la nne kwa wingi…ni vema tufanya kazi kwa bidi na tujitadi kuondoa sifuri na kupunguza Daraja la nne mkoani kwetu” alisisitiza.

Alisema kuwa uwezo wa kuondoa sifuri na kupunguza Daraja la Nne upo kwa kuwa Shule ambazo wanafunzi wanafanya vizuri katika mitihani yao ya mwisho wanafundishwa na walimu sawa na wale walio Tabora na wamepata Mafunzo ya ualimu katika vyuo vil vile ambavyo walimu wa Tabora walipitia.

Makungu alisema walimu wakafanyakazi kwa bidii ili kuongeza idadi ya Shule za Msingi na sekondari nyingi zinazofanya vizuri ikiwemo kuingia katika kumi bora kitaifa na kuufanya Mkoa wa Tabora kutoka namba nane kuwa kwenye tatu bora Kitaifa.

Mwenyekiti wa umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari (TAHOSA) mkoani Tabora Penina Shani aliupongeza Uongozi wa Mkoa wa Tabora kwa kampeni yao inayoendelea ya kuondoa Daraja la sifuri na la nne.

Alisema hatua hiyo imesaidia baadhi ya Shule kushika nafasi za juu kitaifa ikiwemo Shule ya Wavulana ya Tabora ambayo imekuwa ya tano kitaifa katima matokeo ya kidato cha Sita.

Shani alisema kupitia TAHOSA Mkoani wameendelea kushirikiana na Serikali katika kuboresha elimu na kuongeza ufaulu kwa ngazi zote.

No comments:

Post a Comment

Pages