HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 22, 2019

WANAWAKE ZAIDI YA 1000 KUSHIRIKI TAMASHA LA JINSIA

MTANDAO wa Jinsia Tanzania (TGNP Mtandao) umeandaa Tamasha la Jinsia ambalo litafanyika kuanzia Septemba 24 hadi 27, mwaka huu. 

Tamasha hilo ambalo litakuwa la 14, litafanyika katika viwanja vya TGNP Mtandao vilivyopo Mabibo jijini Dar es Salaam, huku wanawake zaidi ya 1000 wakitegemewa kuhudhuria. 

Akizungumzia tamasha hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao, Lilian Liundi alisema tamasha hilo litakwenda sambamba na kuangalia miaka 25 ya harakati za ukombozi wa wanawake nchini.
 
Alisema katika tamasha hilo, kutakuwa na mijadala mbalimbali pamoja na kuangalia miaka 25 tangu lilipotolewa azimio la Beijing. 

"Pia tutasherehekea miaka 25 ya TGNP pamoja na kuadhimisha miaka 25 ya mpango kazi wa Beijing kutafakari ni wapi tulipotoka na tulipo, na nini kifanyike ili tuweze kusonga mbele," alisema Liundi. 

Kwa upande wake Ofisa Mwandamizi wa Programu ya ujenzi wa nguvu za pamoja kutoka TGNP, Anna Sangai alisema
bado jamii inapaswa kupewa elimu zaidi kuhusu mila na desturi potofu kwani masuala ya jinsia hayawezi kufikiwa kama bado chagamoto hizo zipo.

"Hatuwezi kufikia masuala ya kijinsia kama bado hivi vitu vinaendekezwa. Kuna uhitaji mkubwa wa watu kufahamu masuala ya jinsia," alisema Sangai.

No comments:

Post a Comment

Pages