HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 08, 2019

BUKOBA YAKAMILISHA MAANDALIZI YA MITIHANI YA DARASA LA SABA 2019

Mwenyekiti wa Halmshauri ya Wilaya ya Bukoba mkoani Kagera Mhe. Hashim Ngeze akizungumza na waandishi wa habari.


Na Lydia Lugakila Kagera
 Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba Mkoani Kagera imefanikiwa kwa asilimia 98 kukamilisha maandalizi ya Mtihani kwa wahitimu wa darasa la saba 2019 unaotarajiwa kufanyika  Septemba 11-12 Mwaka huu.
Kauli hiyo imetolewa Septemba 7, 2019, na Mwenyekiti wa Halmshauri ya Wilaya ya Bukoba mkoani Kagera Mhe. Hashim Ngeze wakati akizungumza na vyombo vya habari  katika ofisi za halmashauri hiyo zilizopo mkoani hapa.
Ngeze amesema hadi  sasa Mitihani hiyo tayari imeishawasili wilayani humo  na zoezi la kuingawa kwenda shule  za msingi ili kila shule iweze kuipata mitihani yake ambapo pia  kiasi cha fedha kwa ajili ya kusimamia  mitihani hiyo  tayari kimeletwa na bajeti imeishakuwa tayari maandalizi yako vizuri na kutaja maandalizi hayo kufikia asilimia 98.
Mhe. Ngeze amesema Halmashauri hiyo ina  shule 141 za kiserikali na 8 za binafsi huku akitaja  jumla ya wanafunzi ambao wanatarajia kufanya mitihani wilayani humo kuwa wasichana ni 3511 na wavulana ni 3351.
amesema anatarajia  matokeo mazuri sana kwa kuwa  hivi karibuni  serikali imetoa pikipiki kwa waratibu wa elimu kata kwa hiyo ufuatiliaji wa shule ya msingi unaenda vizuri  ambapo amedai kuwa hata kwa mitihani ya ndani wa shule ya msingi kujipima wanafunzi walifanya vizuri kutokana na usimamizi mzuri.

‘’Wito wangu kwa wazazi na walezi wa watoto wanaotarajia kufanya  Mtihani huo ni kuwa karibu na watoto kuwaliwaza,ili wasiwe na mawazo wakiwa ndani ya Mtihani kwa sababu kushindwa kwa mtihani kunaanzia na maandalizi ya mtoto kutoka nyumbani anapoingia ndani ya chumba cha Mtihani ana mawazo jambo hilo linalosababisha kushindwa kufuata maelekezo  ya mtihani, kwa hiyo wazazi kwa kipindi hiki toeni uhuru kwa watoto wenu na mkawape ushauri wa jinsi ya kutulia na kufanya mitihani yao vizuri,,’’amesema.
Amesema kuwa kumekuwepo na tabia ya baadhi ya wazazi wanaowashinikiza watoto wao wasifanye vizuri mitihani yao ili kushinda kuingia kidato cha kwanza kwa sababu ya umbali mrefu wa kufuata shule huku akitolea mfano shule ya msingi Kasharu na Rukoma kuwa hilo limekuwa likifanyika.

Ameongeza kuwa alitembele shule ya msingi Kamukore kati ya wanafunzi 19 wanafunzi 7 walikiri kwamba wazazi wao wameishawaambia wasifanye vizuri mtihani wao wa darasa la saba kwa sababu ya ukosefu wa shule ya sekondari  amewataka wazazi kutolipa kipaumbele suala hilo ili watoto wao wapate elimu sitahiki na kutimiza ndoto zao.
Amesema  zaidi ya shilingi milioni  600 zimepokelewa kutoka serikali ili kuwezesha elimu bila malipo na kumshukuru Rais Dokt. John Magufuli kwa kuanzisha utaratibu wa elimu bila malipo kwa sababu inaondolea wazazi mzigo wa kulalamika.

No comments:

Post a Comment

Pages