HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 15, 2019

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AMUWAKILISHA RAIS DKT. MAGUFULI KUAGA MWILI WA MZEE MUGABE


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwasili nchini Zimbabwe kuhudhuri mazishi ya kitaifa ya aliyekuwa Rais wa Zimbabwe marehemu Robert Mugabe aliyefariki wakati akipatiwa matibabu nchini Singapore wiki iliyopita.




Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisaini kitabu cha maombolezo.
Jeneza la Robert Mugabe.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akitoa salamu za rambirambi wakati wa mazishi ya kitaifa ya Marehemu Mzee Robert Gabriel Mugabe katika Uwanja wa Taifa wa Michezo jijini Harare Zimbabwe.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa na Rais Mstaafu wa Zambia Mhe. Keneth Kaunda na Rais Mstaafu wa Nigeria Mhe. Olubagan Obasanjo wakiteremka kwenye Jukwaa baada ya kutoa Heshima za Mwisho mbele ya Jeneza lenye Mwili wa Rais wa Zamani na Muasisi wa Taifa la Zimbabwe Marehemu Mzee Robert Gabriel Mugabe katika Uwanja wa Taifa wa Michezo jijini Harare Zimbabwe. Makamu wa Rais amemuwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwenye Hafla hiyo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiambatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro baada ya kutowa Heshima za Mwisho mbele ya Jeneza lenye Mwili wa Rais wa Zamani na Muasisi wa Taifa la Zimbabwe Marehemu Mzee Robert Gabriel Mugabe katika Uwanja wa Taifa wa Michezo jijini Harare Zimbabwe. Makamu wa Rais amemuwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwenye Hafla hiyo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Rais wa Ethiopya walipokutana wakati wa Hafla ya kutowa Heshima za Mwisho mbele ya Jeneza lenye Mwili wa Rais wa Zamani na Muasisi wa Taifa la Zimbabwe Marehemu Mzee Robert Gabriel Mugabe katika Uwanja wa Taifa wa Michezo jijini Harare Zimbabwe. Makamu wa Rais amemuwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwenye Hafla hiyo.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Rais Kenya Mhe. Uhuru Kenyata walipokutana wakati wa Hafla ya kutowa Heshima za Mwisho mbele ya Jeneza lenye Mwili wa Rais wa Zamani na Muasisi wa Taifa la Zimbabwe Marehemu Mzee Robert Gabriel Mugabe katika Uwanja wa Taifa wa Michezo jijini Harare Zimbabwe. Makamu wa Rais amemuwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwenye Hafla hiyo. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais).

No comments:

Post a Comment

Pages