HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 21, 2019

MAKATIBU WA CCM KAGERA WASAIDIWA KOMPYUTA

Mbunge wa Vijana Mkoa wa Kagera, Halima Bulembo, akimkabidhi Printa 10 na Kompyuta 10 kwa ajili ya Makatibu wa Wilaya 8 wilayani Muleba.
Katibu wa CCM Mkoa wa Kagera, Raheli Ndegereki (kulia), akipokea msaada kutoka kwa mbunge wa vijana, Halima Bulembo.


Na Lydia Lugakila, Bukoba

Mbunge   wa Vijana  CCM Mkoa wa Kagera, Halima Bulembo amekabidhi Printer 10 na Kompyuta 10 kwa makatibu wa wilaya 8 wa mkoa huo ili kuunga mkono shughuli za chama hicho kufanyika bila vikwaz0.
  
Mhe. Bulembo amekabidhi vifaa hivyo Septemba 20,2019 katika ofisi za chama hicho zilizopo katika manispaa ya Bukoba mkoani Kagera ikiwa ni kuunga mkono shughuli za chama hicho kusonga mbele na kuwesha wanachama wa chama hicho kutenda kufanya kazi za chama hicho bila kuwa na changamoto.

Akiwa Manispaa ya Bukoba mbunge huyo amemkabidhi  printer moja na computer moja ofisi ya mkoa huku akihaidi kuendelea kutoa ushirikiana kwa viongozi hao pamoja na kuwaunga mkono vijana.

Katibu wa CCM Mkoa, Raheli Ndegereki, ameahidi kutumia vifaa hivyo vizuri kwa shughuli za chama huku akimpongeza mbunge huyo.

Hata hivyo viongozi hao akiwemo katibu wa mkoa wa Kagera vijana Salum Suleiman Tate na Katibu wa wilaya vijana wilayani Muleba Athuman Sagara wamefurahishwa na suala hilo na kuwataka viongozi wengine kuwa mfano bra.

No comments:

Post a Comment

Pages