HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 20, 2019

Tigo yajipanga kufika kila kona

Mkurugenzi Mkuu wa Tigo Tanzania, Simon Karikari, akizungumza na waandishi wa habari.

NA SULEIMAN MSUYA
KAMPUNI ya Tigo Tanzania imesema inaendelea kupanua wigo wa huduma zake kwenye maeneo ya vijijini ili kuchochea ukuaji wa uchumi, maendeleo na mawasiliano nchini.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Mkuu wa Tigo Tanzania Simon Karikari wakati akiwasilisha mada kwenye mkutano wa Mawaziri wa Sekta ya Tehama, Habari, Uchukuzi na Hali ya Hewa kutoka nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), ulimalizika jijini Dar es Salaam.
Karikari alisema Tigo imefikia asilimia 90 ya Watanzania kwa kutoa huduma mbalimbali kama mawasiliano, kifedha na inteneti hali ambayo inasaidia jamii kuwasiliana kwa urahisi.
“Nimewaeleza waheshimiwa mawaziri kuwa tumefanikiwa kufikia Watanzania kwa zaidi ya asilimia 90 kwa sasa Tigo ni ya pili kwa hapa nchini kwa kutoa huduma bora,” alisema.

Alisema mikakati yao ni kuhakikisha nafasi ya pili ambayo wanashika kwa kutoa huduma za simu nchini inabakia na baadae kuja kuwa viongozi kwa utoaji wa huduma hizo nchini.
Aidha, alisema mikakati yao itafanikiwa kwa haraka hasa kutokana na mchango wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), kutumia ruzuku wanayopata kupitia makampuni ya simu kusambaza mikonga ya mawasiliano nchini.
Alisema kinachofanywa na UCSAF kwa kutoa ruzuku kinapaswa kuigwa na nchi za SADC ili kuhakikisha huduma ya mawasiliano inatakapaa kila kona ya nchi wanachama kama ilivyo Tanzania.
Mkurugenzi huyo alisema iwapo mfumo wa UCSAF ukipata nafasi katika nchi nyingine ni dhahiri mitandao ya simu katika nchi hizo itasambaa kama Tigo ilivyo samba.
Kwa upande wake Mtaalam wa Uhusiano wa Huduma za Wateja Tigo Business, Joachim Chuwa alisema wao wanaendelea kubuni teknolojia mbalimbali ili huduma za mawasiliano iwe na wigo mpana.
Chuwa alisema hivi sasa wamekuja ubunifu wa tekonolojia inteneti ya kisasa ya ‘Home Inteneti na Ofice Intenet’ ambazo zimeanza kufanya vizuri katika soko.

No comments:

Post a Comment

Pages