HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 08, 2019

VIJANA 774 WAHITIMU MAFUNZO YA UKAKAMAVU 845 KJ.WAKITAKIWA KUTOYATUMIA VIBAYA MAFUNZO HAYO

Na Ibrahim Yassin, Songwe
 
VIJANA 774 wamehitimumafunzoyaukakamavukatikakambiyajeshikikosi cha 845 KJ kilichopo Kata ya Itaka wilayani Mbozi mkoani Songwe huku wakitakiwa kutoyatumia vibaya mafunzo hayo kwa kufanya fujo badala yake wametakiwa kuwa wazalendo kwa kulitumikiaTaifa hili.
Hii ni mara ya kanza kwa kambi hiyo ya Jeshi la kujengaTaifalililopo kata ya Itaka wilayani Mbozi mkoani Songwe kutoa mafunzo kwa vijana 774 ambao wamehitimu mafunzo yao ya ukakamavu na kupewa nasaa mbalimbali ikiwemo y auadirifu na uzalendo kwaTaifa.
Filimon Mahenmge mkuu wa kambi hiyo alisema vijana hao walianza mafunzo hayo wakiwa 780 kat ya hao wavulana 620 na hivi leo waliohitimu ni 774 kati ya hao wavulana 615 hivyo vijana 6 hawakushiriki mafunzo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ya utoro.
Alisema vijana hao wameiva vizuri ndani ya miezi mitatu hivyo anaamini huko watako kwenda watakuwa ni mabarozi wazuri katika kulitumikia Taifa na kuwa wazalendo kwa nchi yao na hata watakaoendelea na masomo vyuoni watafanya vyema zaidi.
Anchilla Kagombola muwakilishi wa mkuu wa jeshi la kujenga Taifa nchini,alisema ni kuu ya serikali kupitia Jeshi la kujenga Taifa ni kuwakusanya vijana pamoja na kuwafundisha mbinu za kijeshi pamoja na ukakamavu  na kuwajenga kimaadili ili waweze kulitumikia Taifa hili la uadirifu.
John Palingo mkuu wa wilaya ya Mbozi aliyekuwa mgeni rasmi katika ufungaji wa mafunzo hayo ,amewaasa wahitimu hao kutoyatumia vibaya mafunzo waliyo yapata kwa kufanya vurugu mitaani na badala yake wametakiwa kuyatumia vyema kwa kuwa waadilifu na kioo kwa jamii.
Alisema adui namba moja wa serikali hii ni rushwa,ufisadi na mambo mengine maofu,hivyo anaamini mafunzo waliyoyapata vijana hao wataenda kupingana na vitendo hivyo na ndiyo maana muasisi wa Taifa Mwl ,Julius Nyerere aliamua kuanzisha kitengo hiki kwa ajili ya kuwapika kimaadili vijana ili waweze kuwa viongozi bora.
Ayoub Majid mhitimu wa mafunzo,alisema kupitia mafunzo hayo wamejifunza mambo mengi ya ukakamavu na mbinu za kijeshi,hivyo anaamini atauwa barozi mzuri huko aendako na kuwahakikishia viongozi waliowapa nasaa kuwa ushauri wao watautumia vyema.
Njegela Maganda mhitimu wa mafunzo,alisema kutokana na umuhimu wa mafunzo hayo aliiomba serikali kuongeza muda ili waweze kuwa wakakamavu zaidi kwani muda wa miezi mitatu alisema hautosho licha ya kuwa tayari wamepata mafunzo yote muhimu.
Rameck Iromo Mhitimu wa Mafunzo,alisema mafunzo yalikuwa mazuri hivyo aliiomba serikali kutatua changamoto zilizopo kwenye kambi hiyo ikiwemo kusogeza maji karibu,kuongeza nyumba za watumishi pamoja na mabweni ombi ambalo lilikubaliwa na mkuu wa wilaya hiyo.

No comments:

Post a Comment

Pages