HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 03, 2019

WANAOWAPA UJAUZITO WANAFUNZI KUKIONA KAGERA

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba mkoani Kagera, Hashimu Murshid Ngeze. 

Na Lydia Lugakila, Kagera

Wazazi na walezi mkoani Kagera wametakiwa kuacha dhana potofu ya kuwavunja moyo watoto wao hasa wanafunzi wanapokaribia kufanya mitihani ya taifa kwa kuwatamkia neno FANYA VIBAYA MTIHANI  ILI UWEZE KUSHINDWA.
Kauli hiyo imetolewa leo Septemba 3, 2019 na Mwenyekiti  wa Halmashauri ya wilaya ya Bukoba mkoani Kagera Murshid Hashimu Ngeze katika kuelekea kufanya mitihani ya Taifa kwa wanafunzi wa shule ya msingi kote nchini
Ngeze amesema kuwa kitendo hicho cha mzazi au mlezi kumtamkia mwanaye kuwa afanye vibaya mtihani   ili ashindwe ni kikwazo kikubwa  kinachokwamisha juhudi na doto za mtoto katika kufikia malengo yake tarajiwa.
‘’Si vizuri mtoto usimvunje moyo  mwache mtoto afanye vizuri njia ya jinsi mtoto atasoma ni mungu anayejua sisi Halmashauri tupo tunajua ni jinsi gani mtoto atapata Elimu amesema.’
Mwenyekiti huyo ameongeza kuwa baadhi ya wazazi wamekuwa na tabia ya kutoongea na watoto wao hasa mabinti katika misingi iliyo bora, hivyo amewahimza wazazi na walezi  kununua vifaa muhimu vya watoto ili kunufaika na  Elimu bure iliyoko hapa nchini.
Amesema ni muhimu sana   wazazi na walezi kukaa na watoto wao wa kike kuwafundisha jema na baya ili waweze kukua ki maadili.
Katika hatua nyingine Ngeze amekemea tabia za baadhi ya waendesha pikipiki maarufu kama boda boda wanaowadanganya wanafunzi kwa kuwarubuni kwa  zawadi na lifti, kuwa tabia hiyo sio nzuri ambapo tayari mikakati mbali mbali inafanyika ili kupambana na vitendo hivyo ambavyo huwafanya wanafunzi kukatisha masomo kwa kupata ujauzito na kushinddwa kufikia malengo yao.
Amewataka wanafunzi wilayani humo kufanya mtihani wao vizuri unaotarajiwa kufanyika  wiki ijayo  Septemba kumi na moja na kumi na mbili mwaka huu bila kuwa na vikwazo vya kusingizia kufuata shule umbali mrefu kwani tayari ujenzi wa shule unaendelea  wilayani humo.
Aidha ametoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dokta John Magufuli kwa kitendo cha kuwaita ikulu watendaji wa kata kote nchini kwa lengo la  kuzungumza nao kwa kuwapa maelekezo ya kuijenga nchi.
Akigusia sualala maendeleo amesema kuwa katika utawala wa Rais Magufuli vijiji 94 katika halmashauri hiyo kila mwaka  kijiji  kimoja kitakuwa kinapata elfu 45 katika uendeshaji wa maendeleo kwenye vijiji hivyo.
Ametaja hatua hiyo kuwa kubwa kuwa ni kutokana na juhudi za Rais Magufuli na kudai kuwa halmashauri hiyo haijawahi  kugusa fedha za maendeleo na kuziweka katika shughuli za kawaida.
Ikumbukwe kuwa Halmashauri hiyo ina kata 29 vijiji 94 na katika vijiji vyote hivyo vina miradi mbali mbali inayoendelea  miradi hii ipo katika makundi matatu ambayo ni miradi ya serikali kuu,miradi ambayo inatoa fedha kutoka mapato ya ndani na miradi ambayo ni ya wahisani kwa ushirikiano na wananchi.
Mwenyekiti huyo amewataka  wananchi kushiriki katika  miradi mbali mbali ya kimaendeleo  kwa ukamlifu na kuguswa na miradi hiyo  ambapo hadi sasa ameitaja Halmashauri hiyo kuwa  katika hatua nzuri kwani miradi mingi inaendelea kutekelezwa ambapo usimamizi wa fedha ni mzuri pia.
Hata hivyo amesema  kuwa serikali hutumia fedha nyingi katika miradi ya maendeleo kwa wananchi hivyo ni vema  miradi hiyo itunzwe  na kuilindwa.
 Na kuwataka wananchi  kutoa taarifa  mara moja pale wanapogundua au kubaini  baadhi ya watu wanaohujumu miradi hiyo ili hatua kali ichukuliwe.
Taarifa za ukaguzi mbali mbali zimekuwa zikifanyika ikiwemo ya CAG au ukaguzi wa ndani hama wakaguzi kutoka mkoani ambapo mara nyingi wamekuwa wakiikagua na pale ambapo wamekuwa wakikuta mapungufuwamekuwa  wakishauri.

No comments:

Post a Comment

Pages