HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 05, 2019

Aga Khan yawafanyia uchunguzi Wagonjwa 835

Daktari wa mionzi ya nyuklia kutoka Hospitali ya Aga Khan Dk. Raghu, akimuhudumia mgonjwa katika mashine ya kisasa ya mionzi ya nyuklia yenye uwezo wa kufanya uchunguzi wa magonjwa ya saratani, figo, moyo na ubongo. (Na Mpiga Picha Wetu).
 

NA JANETH JOVIN
 
JUMLA ya watu 835 wamefanyiwa uchunguzi wa magonjwa katika Hospitali ya Aga Khan kwa kutumia mashine ya kisasa ya mionzi ya nyuklia (Spect Gamma Camera), ambao inauwezo wa kugundua mapema matatizo yanayowasumbua mtu na kwa kiasi gani yameenea mwilini.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Tiba na Mkuu wa Idara ya Ladiolojia wa hospitali hiyo, Dk. Ahmed Jusabani amesema asilimia 99 ya wagonjwa yaliochunguzwa ni ya mifupa, figo, moyo, mfumo wa mkojo pamoja na saratani zote ikiwamo ya matiti na shingo ya kizazi.

Amesema uwepo wa mashine hiyo imeisaidia hospitali kuweza kuwatambua wagonjwa wenye matatizo na kuwapatia huduma bora kwa haraka kabla ya tatizo alijaenea mwilini.

Jusabani amesema hospitali hiyo ya Aga Khan kwa kushirikiana na Kampuni ya Siemens imeweza kuwa hospitali ya kwanza binafsi Tanzania kuwekeza katika kutoa huduma hiyo ya mionzi ya nyuklia hivyo kuwawezesha watanzania kupata huduma bora hapa nchini pasipo kwenda nje ya nchi kufuata tiba.

“Mashine hii imekuwepo hospitali hapa kwa miaka mitano sasa na imekuwa msaada kwa wagonjwa wengi ambao wameanza kuwa na dalili za saratani na magonjwa mengine.

Teknolojia iliyopo kwenye mashine inauwezo wa kugundua magonjwa mapema zaidi na kuona yameenea sehemu ya mwili kwa kiasi gani, pia kugundua tiba anayopatiwa mgonjwa kama inafanya kazi au la,” amesema na kuongeza.

“Nisisitize kuwa mashine hii haitumika kwa magonjwa ya kansa tu bali inatumika kwa magonjwa mengine yasikuwa ya saratani, na inatumiwa na watu wazima hata watoto wachanga pia wanaweza kufanyiwa kipimo kwa kutumia mashine hii,” amesema.

Naye Daktari Bingwa wa Mionzi ya Nyuklia nchini, Dk. Tausi Maftah amesema mionzi hiyo ya nyuklia inauwezo wa kutambua magonjwa katika hali ya awali hivyo kumsaidia mgonjwa kufanya matibabu na kupona kabisa.

Hata hivyo amesema changamoto iliyopo ni uwepo wa idadi kubwa ya watu wanaotaka kufanya vipimo vya saratani lakini wanashindwa kutokana na uchache au kukosekana kabisa kwa mashine hizo katika hospitali zingine.

“Mpaka sasa mashine za mionzi nchi nzima zipo tatu tu, yaani hapa Aga Khan, Ocean road na Bugando Mwanza, ukiangalia hii utaona jinsi ambavyo bado tunahitaji kuwa na vifaa hivi katika hospitali nyingine ili wananchi waweze kupima na kupata huduma,” amesema.

Kwa upande wake Mtaalamu wa mionzi kutoka Marekani katika  Chuo cha Albert Binsten, Dk. Tony Abraham amesema ni muhimu mashine hiyo ikawepo nchini kwa wingi kwani inawasadia madaktari kufanya uchunguzi kwa usahihi na kwa mgonjwa kupata matibabu kwa haraka.

No comments:

Post a Comment

Pages