HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 19, 2020

DC TABORA ATOA SIKU SABA HALMASHAURI KUWEKA VIBAO VYA UPIGAJI MARUFUKU UTUPAJI TAKA OVYO

NA TIGANYA VINCENT
 
MKUU wa wilaya ya Tabora Komanya Kitwala ametoa siku saba kwa Afisa Mazingia wa Manispaa ya Tabora kuhakikisha ameweka vibao vinavyozuia utupaji wa takataka katika maeneo ambayo sio rasmi ili sehemu ya kuzuia uchafuzi wa mazingira.

Alisema kutokewepo kwa vibao hivyo kumesababisha baadhi ya watu kutupa taka hata katika maeneo ambao sio rasmi na kusababisha kuzagaa kwa taka na kuhatarisha afya za wananchi.

Kitwala ametoa kauli hiyo juzi wakati wa kikao cha Kamati ya Ushauri ya Manispaa ya Tabora cha kupitia mapendekezo ya bajeti ya mwaka 2020/21.

Alisema baada ya kuweka vibao ni vema wakaweka Askari wa Jeshi la Akiba ambao hawana sare kuwavizia wale wote wanaokaidi agizo la kutotupa taka ovyo na kuwakamata ili watonzwe fedha kulingana na maagizo ya Sheria ndogo ndogo za Halmashauri.

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya aliuagiza uongozi wa Manispaa ya Tabora sehemu ya mazingira kuhakikisha wanaongeza vifaa vya kuweka taka katika maeneo mbalimbali ya Manisapa ya Tabora ili kuondoa visingizio kwa baadhi ya watu wanaotupa taka ovyo kwa madai hakuna vifaa vya kuwka taka mitaani.

Kwa upande wa Mazingira wa Manispaa ya Tabora William Mpangala alisema zoezi la kuandaa vibao vya matangazo ya kupiga marufuku utupaji wa taka katika maeneo yasiyo rasmi limeshaanza na wanatarajia ndani ya mwezi huu kuvisambaza katika maeneo mbalimbali.

No comments:

Post a Comment

Pages