NA TIGANYA VINCENT
HALMASHAURI ya Wilaya ya Igunga imependekeza ya makisio ya mapato na matumizi
ya zaidi shilingi bilioni 45.9 kwa ajili
ya mwaka ujao wa fedha wa 2020/21.
Fedha hizo
zinatarajia kutokana na makusanyo ya vyanzo mbalimbali ikiwemo ruzuku toka
Serikali kuu na makusanyo yanayotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri.
Kauli
hiyo imetolewa jana na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilya ya
Igunga Joel Nkesela wakati wa kikao na Sekretaieti ya Mkoa wa Tabora cha
kuchambua na kujadili
mapendekezo ya makisio ya mipango na
bajeti za Mamlaka ya Serikali za Mitaa kwa mwaka ujao wa fedha wa 2020/21.
Alisema kati ya fedha hizo bilioni 42.7 ni
ruzuku kutoka Serikali kuu na bilioni 3.1
zitatokana na makusanyo yanayotokana na
mapato ya ndani.
Nkesela
alisema mapendekezo ya bejeti ijayo yamezingatia uimarishaji wa makusanyo
ya ndani kwa kutumia mfumo wa kielektroniki na kuongeza vyanzo vya mapato vipya
ili kuongeza mapato.
Aliongeza
kuwa vipaumbe vingine ni pamoja kuboresha huduma za afya na elimu ya awali hadi
kidato cha nne na kuimarisha miundombinu ya utoaji elimu na lishe kwa watoto
wenye umri wa chini ya miaka mitano.
Nkesela
alisema pia wanakusudia kuendeleza kilimo cha mpunga kwa kuimarisha miundombinu
ya umwagiliaji na utoaji wa huduma za ugani kwa wakulima ili kuongeza
uzalishaji wa zao hilo.
Naye Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Hamis
Mkunga aliwataka viongozi wa Halmashauri hiyo kujitahidi kubuni na kuimarisha
vyanzo vipya wa mapato ili wawe na uwezo
wa kujitegemea ifikapo mwaka 2025 kama Serikali ilivyoagiza.
Alisema
sanjari na hilo ni vema wakaanza kutenga fedha katika bajeti yao kwa ajili ya ununuzi ardhi ambayo wataipima kwa ajili ya uwekezaji
wa aina mbalimbali ambao utawasaidia kwenye uongezaji wa mapato kwa Halmashauri
na pia kutoa ajira kwa wananchi.
Mkunga
alisema miaka imebaki michache kufika 2025 ni vema wakaongeza kazi katika
mipango yao ya kuwa na vyanzo vya mapato vingi ambao vitawasaidia kupata fedha
za uendeshaji wa shughuli mbalimbali za Halmashauri ikiwemo kulipa mishahara ya
watumishi.
Kwa
upande wa Katibu Tawala Msaidizi Mkoa wa
Tabora Rukia Manduta alizitaka Halmashauri zote ikiwemo Igunga ambazo haziwalisha
andiko la miradi ya Kimkakati kuandika haraka ili waweze kuomba fedha ambazo
zitawasaidia katika utekelezaji wa mradi waliopanga kwa ajili ya kujiongezea mapato
yao ya ndani pindi utakapokuwa umekamilika.
No comments:
Post a Comment