HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 22, 2020

IFC LAIPIGA TAFU TMRC

Mkurungenzi Mkuu wa Shirika la Fedha IFC, Frank Ajilore, akizungumza, na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam. (Na Mpiga Picha Wetu).


NA FARAJA EZRA
BENKI ya Dunia  kupitia  kupitia Shirika la Fedha (IFC) na Kampuni ya Mikopo ya Nyumba  Tanzania( TMRC) zaingia Ubia kuendeleza upatikanaji wa mikopo ya Nyumba  za Makazi yenye gharama nafuu.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo  Frank Ajilore, alisema IFC limewekeza kiasi cha dola za kimarekani milioni 5. 75 sawa na shilingi bilioni 13.3 kwaajili ya kuwezesha ukuaji wa soko la mikopo ya Nyumba  za Makazi nchini.

Aidha kuwawezesha jamii kupata Makazi bora lakini pia upatikanaji wa  Nyumba  za Makazi za gharama nafuu.

Alisema uwekezaji huo unahusisha  Shirika la la IFC kununua hisa za TMRC zenye thamani ya  don'tola  milioni 1.5 na kuwekeza milioni 4.25 zitakazowezesha  Kampuni ya mikopo kutoa hati fungani kwenyev soko la mitaji kwa muda wa miaka mitano.

Alisema  IFC imejipanga  kuwezesha  ukuaji wa soko la nyumba nchini kwa kuwezesha  upatikanaji wa fedha ilinkuongeza  Kasi ya ukuaji wa  soko la nyumba za gharama nafuu.

Naye Makamu Mwenyekiti wa  bodi ya TMRC Alieleza kuwa TMRC ni Taasisi ya kifedha  iliyoanzishwa mwaka 2010 ikiwa ni  moja ya utekelezaji wa mradi wa Serikali uliofadhiliwa na benki kuu ya Tanzania na iliwezesha mikopo ya milioni 70 kwa ajili ya kutoa mikopo kwa wateja kupata makazi bora.
Huku  IFC ni Taasisi ya kibenki ambayo hujishughulisha na maendeleo ya sekta binafsi kwenye  nchi za uchumi unaoendelea.
 

" Hadi sasa  TMRC  imeshatoa mikupuo miwili ya hati fungani yake yenye thamani ya shilingi bilioni 21.7 na kuioroshesha kwenye soko la hisa la Dar es Salaam na kupunguza  utegemeza kwa pesa za umma" alisema  na kuongeza.

"Uwekezaji huu wa IFC  utawezesha TMRC kuvutia wawekezaji wengine wapya  kwenye hatifungani yake nabhivyo kuwezesha  Kampuni ya mikopo ya nyumba  kupata Fedha za muda mrefu" alisema.

Hata hivyo alisema Uwekezaji huo umejikita  katika maeneo mbalimbali ikiwemo, ujengaji wa uwezo kwenye masoko ya Nyumba , utoaji wa elimu kwa umma kuhusu mikopo ya nyumba , kujenga uwezo wa benki zinazotoa mikopo ya nyumba na  namba Bora ya kutoa mikopo.

No comments:

Post a Comment

Pages