HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 04, 2020

PROF. MUHONGO KUONGOZA HARAMBEE

Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo  amepanga kuongoza harambee ya kuchangia fedha za kujengea vyumba vya madarasa 13 katika shule  zenye ufungufu jimboni humo.

Katika harambee hiyo Prof. Muhongo atawashirikisha wanavijiji mbalimbali ili kutimiza lengo la kunusuru hali hiyo itakayookoa wanafunzi 616 wanaotarajia kujiunga Kidato cha Kwanza mwaka huu katika shule hizo zenye upungufu wa vyumva vya madarasa.

Mbunge Muhongo anataajia kutembelea shule zote za sekondari zenye upungufu huo na hatimaye kuandaa harambee ya kuwezesha ujenzi wa vyumba hivyo haraka iwezekanavyo ili wanafunzi wasikose kujiunga.

“Shule zinafunguliwa Jumatatu, tarehe 6.1.2020, bado tunao upungufu wa vyumba 13 vya Madarasa ya Kidato cha Kwanza (Form I).
Vyumba 13 hivyo visipopatikana wanafunzi 616 watabaki nyumbani wakisubiri uwepo wa  Vyumba vya Madarasa yao,” alisema Prof. Muhongo hivi karibuni jimboni humo.
.
Ameanza kutembelea shule hizo leo na kuona kila shule vyumba vilivyopungua.

No comments:

Post a Comment

Pages