HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 18, 2020

Serikali; Walemavu wasio na mikono, vidole wanasajilije simu? Kwa vidole vya miguu!!

Na Bryceson Mathias
WAKATI zoezi la kusajili simu kwa alama za vile liendea ukingoni! Wananchi, Ndugu, na baadhi ya walemavu wasio na Vidole wameilalamikia Serikali kuu wakihoji changamoto ya walemavu wasio na vidole, wanasajili namna gani simu kwa alama za vidole?.
Aidha wameonesha wasiwasi wao kutokana na usajili huu wa ‘Mwendo Kasi’ kwamba, Taifa linaweza likaruhusu wageni kujipenyeza mpaka chumbani kwa sababu rushwa ikitumika kutafuta fursa hii adimu, maana hata wasio raia wanaitumia ili kufaidi keki hii.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wenye ndugu wasio na mikono au vidole vya mikono kwa sababu ya maradhi au madhira tofauti tofauti wamedai, baadhi yao wamefanya kinyume kwa kusajili simu za walemavu hao kwa kutumia majina na vidole vya ndugu zao isivyo sahihi! Je Serikali inasemaje?
“Waliosema ukweli wakiomba kuwasajilia simu zao kupitia majina ya wenye viungo walikataliwa na watendaji! Je kwa msingi huo watasajilije simu zao au serikali itatoa mwongozo mwingine juu ya wenye ulemavu huo?”.alihoji mwananchi mmoja ambaye aliomba asitajwe.
Mmoja wa Wakazi alisema,”Nalisaidia Taifa langu, wageni ambao wana uchu wa fursa za Tanzania za kupata Ardhi, Makazi, Huduma za Kijamii, Kazi, Ufugaji, Uvuvi, Kilimo na shughuli zingine za kijamii nchini, wanatumia mwanya huo na wengine wanafanikiwa kupenya”.
Hata hivyo katika Kipindi cha Mjadala wa Tuongee Magazti 18/01/2020, Mwandishi Mkongwe, Jacton Manyerere, naye alilalama na kushauri kuwa, Waandishi, Watawala watambue wageni wana uchu na fursa ya Amani ya Tanzania ambapo mtu unaweza kukaribishwa kula usuhojiwe.
Alisema kuna minong’ono katika baadhi ya maeneo ya wafugaji na utalii ikiwemo nchini, wapo baadhi ya wageni wamejipenyeza kuanza kusaka usajili huo wa mwendo kasi kwa udi na uvumba ili wafaidi matunda hayo akidai watatumia hata rushwa na kufanikiwa ukikosekana umakini, akisisitiza kuchelewa usajili si kosa la wananchi tu!.
Mbali ya Manyrere, Mwandishi, Peter Saramba, alisema uwezekano wa kusajili simu kwa wakati (meet target) kwa siku mbili zilizobakia itakuwa ni ndoto, ila anaamini Serikali na Rais John Magufuli kupitia kwa washauri wake, atakuwa ameona changamoto hiyo, hivyo huenda akaongeza muda kukidhi changamoto hata za walemavu wasio na vidole na mikono.  

No comments:

Post a Comment

Pages