Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Komanya Kitwala (wa pili kushoto), akifungua jana kikao cha Kamati ya Ushauri ya Manispaa ya Tabora (DCC) ya kupitia na kujadili makisio ya mapendekezo ya mpango na bajeti ya shilingi bilioni 52 kwa ajili ya mwaka wa fedha ujao. (Picha na Tiganya Vincent).
Na Tiganya Vicent
WAJUMBE
wa Kamati ya Ushauri ya Manispaa ya Tabora (DCC) wamepitisha makisio ya
mapendekezo ya mpango na bajeti ya shilingi bilioni 52 kwa ajili ya mwaka wa fedha ujao wa fedha.
Wajumbe
hao walipitisha mapendekezo hayo jana baada ya Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa
ya Tabora Bosco Ndunguru kuwasilisha wakati wa kikao kupitia mapendekezo ya
bajeti ya mwaka 2020/21.
Alisema
katika mapendekezo hayo wanatarajiwa kukusanya shilingi bilioni 4.7 kutokana na
mapato ya ndani ya Halmashauri ikiwa ni ongezeko la asilimia moja ukilinganisha
na masikio ya mwaka 2019/20 ya kukusanya bilioni 4.6.
Ndunguru
alisema kwa upande wa Serikali Kuu na kwa wahisani wanatarajia kupata jumla
shilingi bilioni 48 ikiwa ni ongezeko la asilimia 25 ukilinganisha na bilioni 38.2
ya mwaka 2019/20.
Alivitaja
vipaumbele vya bajeti ijayo kuwa ni uendelezaji wa jengo la utawala ambalo
limetengewa milioni 200, kutenga fedha milioni 70 kwa ajili ya ununuzi wa ardhi
ekari 140 za uwekezaji.
Nduguru
aliongeza kuwa vipaumbele vingine ni kutenga milioni 50 kwa ajili ya fidia kwa
wananchi ili kutatua migogoro, milioni 84 kwa ajili ya uboreshaji wa miundombinu ya Shule za Msingi na Sekondari na ununuzi wa taulo kwa ajili ya
wanafunzi wa kike na milioni 200 kwa ajili ya ujenzi wa Shule mbili za Kidato
cha Tano na Sita.
Aliongeza
kuwa kiasi cha milioni 445 kinatarajiwa kutolewa kama mikopo ya vikundi vya
vijana , wanawake na walemavu na milioni 117 zimetengwa kwa ajili ya shughuli
za lishe.
Ndunguru
alisema kwa upande wa miradi wamependekeza shilingi milioni 580 zitumike katika
miradi ya maendeleo kwenye Kata 29 za Manispaa ya Tabora na bilioni 1 zimetengwa kwa ajili ya miradi ya
maendeleo ya Halmashauri hiyo
No comments:
Post a Comment