HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 23, 2020

TOZO ZA KUHIFADHIA MAITI KUPITIWA UPYA-CHUNYA

NA KENNETH NGELESI, CHUNYA

MKUU wa Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya, Mhandisi Maryprisca Mahundi, ameagiza kupitiwa upya tozo za kuhifadhi maiti katika hospitali ya Wilaya ya Chunya.

Agizo hilo alilitoa katika warsha iliyoandaliwa Baraza la Kikristo Tanzania (CCT) kupitia mradi wa PETS unaojumisha wananchi ngazi ya Kijiji na Kata.

Mratibu wa warsha hiyo Edward Mwasote alisema lengo la warsha huyo ni kuwakutanisha wananchi na viongozi ili kuwasilisha kero zao na serikali  kuzipatia ufumbuzi.


Kwa upande wake Mwezeshaji wa warsha hiyo kutoka CCT Dodoma Wakili Msomi Beatrice Tengeneza alisema warsha hiyo ilikuwa na lengo la kuwawezesha wananchi kukutana na viongozi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwasilisha kero na mafanikio yaliyofanywa na serikali.

Aidha alisema si lazima kupokea kero tu bali hata mafanikio yaliyofanywa na serikali kwa lengo la kuyafikia maendeleo ya pamoja.

Akiwasilisha kero mbalimbali kwa niaba ya wananchi Padre Goodluck Mlelwa alisema hospitali ya Wilaya ya Chunya imekuwa ikitoza tozo kubwa kwa ajilu ya kuhifadhi maiti kwa siku ambapo hutozwa shilingi elfu arobaini kwa siku.


Mlelwa alisema pia tozo kwa wanafunzi wanaojiunga kidato cha kwanza licha ya kuwa na kadi ya bima ya afya.

Naye Wakili Beatrice Tengeneza kwa niaba ya wajumbe alisema wananchi wa Kijiji cha Igodima wamelalamikia  ubovu wa barabara pia kutokuwepo huduma za umeme.

Alisema pia kuchelewa kukamilika kwa zahanati kunazorotesha maendeleo.

Akijibu kero za wananchi kuhusiana na tozo kubwa za kuhifadhi maiti Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhandisi Maryprisca Mahundi alimwagiza Mganga Mkuu Felister Kisandu kuhakikisha wanarekebisha bei hizo kwana chumba hicho cha kuhifadhia maiti kimejengwa na wananchi.

Mahundi alisema wananchi wanapaswa kupata huduma kwa gharama nafuu kuliko awali ambapo wananchi walikuwa wanahidhi maiti Mbeya umbali wa kilometa sabini na mbili.

No comments:

Post a Comment

Pages