HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 22, 2020

Viongozi ACT Pemba Wachiwa kwa dhamana

Na Talib Ussi, Zanzibar
Mwanyekiti wa Mkoa wa Kaskazini Pemba wa chama cha ACT-Wazalendo Rashid Khalid Salim na wazake saba wameachiwa kwa dhamana katika kituo cha Polisi Wilaya ya Micheweni.
Akizungumza na  waandishi wa habari Habari Katibu wa  katiba na sharia pamoja na haki za Binaadamu wa Chama hicho Kombo mwinyi Shehe alisema kuwa watu wao tayari wameachiwa na wametakiwa warudi tena kesho kituoni hapo kwa kukamilisha masharti waliokewa.
Shehe alisema kuwa Jeshi la Polisi limewataka watu hao akiwemo Mwenyekiti  wa ACT mkoa huo kupeleka  mdhamini MMoja na laki Tano za maandishi.
“Alihamdulillah watu tumewapata na sasa tunarudi nao nyumbani kuwapamoja na familia zao na kesho tutarudi tena kukamilisha masharti waliyotuwekea” alieleza Shehe
Waliowekwa ndani ni Rashind Khalid Salim  (57), Abdi Khatib Suleiman (42), Ali Rajab kombo (53) Abdallah Ali Said (48), Ali Said Faki (30)  Hatib Saleh Juma (14) Pamoja na Said Shinei Hamad.
Watu hao walikamatwa tarehe 18 na 19 mwezi huu baada vibanda viwili vya makuti ambao vinamilikiwa na wafuasi wa chama cha Mapinduzi katika Shehia ya Wingwi Mapofu Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Hali imekuja baada ya kuaza kwa uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kuaza Pemba huku wafuasi wa vyama vya Upinzani wakilalamika kunyimwa haki hiyo kutokana kukosa Vitambulisho vya Mzanzibar Mkaazi ambacho kinawapa uwezo wa kufanya  usajili huo

No comments:

Post a Comment

Pages