HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 24, 2020

Wateja Tigo kupiga simu mitandao yote


Kaimu Ofisa Mkuu wa Biashara wa Tigo, David Umoh, akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni mpya iitwayo Ujanja Ni, inayowawezesha wateja kuwa na uwezo wa kupiga simu kwenda mitandao mingine kwa gharama nafuu kupitia huduma zilizoboreshwa zaidi. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko, William Mpinga. (Na Mpiga Picha Wetu).



NA SULEIMAN MSUYA

KAMPUNI ya Tigo imezindua kampeni ijulikanayo kama ‘Ujanja Ni’ ikiwa na lengo la kuwapa wateja thamani ya pesa zao kila wanapotumia bidhaa zao.
Kampeni hii itawapa wateja uwezo wa kupiga simu kwenda mitandao mingine kwa gharama nafuu kupitia huduma zilizoboreshwa zaidi.
“Vifurushi vyote vya sauti vinampa mteja uhuru wa kupiga simu mitandao yote kwa bei ile ile. Huduma hii ni ya kwanza katika soko la simu na ni suluhisho kwa wateja wa Tigo kwa sababu itaweza kubadili namna ambavyo watu wanatumia huduma za mawasiliano  hapa nchini,” ilisema taarifa.
Akizungumzia fursa hiyo wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, Kaimu Ofisa Mkuu wa Biashara wa Tigo, David Umoh huduma hizi zinampa mteja uhuru wa kupiga simu kwenda mtandao wowote kwa gharama ileile.
Alisema wateja wanaweza kununua kifurushi chochote cha dakika, intaneti au vifurushi mchanganyiko na kufurahia faida zote muhimu kwa gharama nafuu zaidi,”
Aidha, alisema vifurushi vyote vimeboreshwa kwa kuongezewa muda wa maongezi, SMS pamoja na intaneti.
Pia alisema huduma hizi zinakuja pamoja na vifurushi vya wiki na mwezi ili kumpa mteja uwezo wa kuwasiliana zaidi, kuperuzi na kupata thamani ya pesa yake katika kila matumizi anayoyafanya.
Umoh alisema kampeni hiyo inaendana na jitihada za Serikali za kuhakikisha huduma za kupiga simu kwenda mitandao yote zinakuwa nafuu.
“Kama kampuni ya kidigitali tunaamini kuwa huduma hii itasaidia kuongeza uhuru wa mawasiliano na kuwaunganisha wateja wetu na wapendwa wao bila mipaka kutoka Tigo kwenda mitandao mingine.
Tunaanzisha huduma hii chini ya kampeni iitwayo ‘Ujanja ni’ ikiwa na maana kwamba ujanja ni kutumia fursa hii ya kupiga simu kwenda mitandao yote ukiwa na Tigo,” alisema Umoh
 “Kwa mara ya kwanza, zaidi ya wateja 12 milioni hawatakuwa na wasiwasi tena pale wanapotaka kuwasiliana na watu waliopo kwenye mitandao mingine hapa nchini. Hii inadhihirisha jitihada zetu za kuwa mtandao ambao unampa mteja thamani zaidi kupitia huduma za kibunifu,” alisema Umoh.

No comments:

Post a Comment

Pages