HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 16, 2020

JAJI SEPETU WA MAHAKAMA KUU ZANZIBAR AFARIKI DUNIA, KUZIKWA LEO KIJIJINI KWAO MBUZINI

Na Andrew Chale, Unguja- Zanzibar

JAJI wa Mahakama Kuu ya Zanzibar Mhe Mkusa Issack Sepetu (pichani), amefariki dunia asubuhi ya leo na mjini hapa.

Kwa mujibu wa taarifa ya Afisa Habari wa Mahakama Kuu Zanzibar, asubuhi ya leo February 16, ilieleza juu ya kifo hicho.

Pia inaelezwa kuwa, maziko yanataraji kufanyika leo saa 10 Kijijini kwao Mbuzini.

Enzi za uhai wake amewahi kushika nyadhifa mbalimbali ikiwemo Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na baadae Kaimu Jaji Mkuu wa Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

Pages