Na Luteni Selemani Semunyu
Mwenyekiti wa Klabu ya Gofu ya Lugalo Brigedia Jenerali
Mstaafu Michael Luwongo ametangaza mashindano ya Tanapa Lugalo Open
yanatarajiwa kufanyika Machi 14 na 15 Mwaka huu katika Viwanja vya Lugalo
Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Mwandishi wa hbari hizi Mwenyekiti huyo
alisema masindano hayo yalikuwa yafanyike February 29 na Machi Mosi lakini kutokana na baadhi ya
Maandalizi kutokamilika imelazimu sasa kusogeza mbele.
“ Tumesogeza mbele ili kutoa fursa ya wachezaji wengi kutoka
maeneo mbalimbali kuweza kufanya maandalizi na kushiriki hasa kwa wachezaji
wanaotoka katika vilabu mbalimbali nje ya Jiji la Dar es salaam ambao walikuwa
wakisubiria kwa hamu kubwa Mashindano hayo.” Alisema Brigedia Luwongo.
Aidha alisema pia Mgeni rasmi katika ufungaji wa Mashindano
hayo anatarajiwa kutangazwa baadae katika mkutanona Waandishi wa habari mara
baada ya kuthibitisha kuwepo katika mshindano hayo kulingana na ratiba zake.
Kwa upande wake Nahodha wa Klabu ya Lugalo Kaptni Japhet Masai alisema tayari taaarifa
zimeshatumwa kwa manahodha wa Vilabu mbali mbali na Dirisha limeshafunguliwa
kwa yeyote anayetaka kushiriki kuweza kujiandikisha.
“ Mpaka sasa tunawachezaji zaidi ya 50 wameshajiandikisha
ikiwa ni siku moja tangu kufunguliwa kwa zoezi la kujiandikisha hali
inayoashiria mashindanohaya kuwa na
mvuto zaidi mwaka huu ukilinganish na mwaka uliopita” alisema Kapteni Masai.
Kwa upande wa Wanawake nahodha wa Timu hiyo kwa Lugalo Hawa
Wanyenche alitoa wito kwa Wanawake katika Vilabu mbalimbali na Nchi za Afrika
Mashariki kujitokeza katika Mashindano hayo ya kwanza Makubwa katika Mwaka huu
tangu vianze.
Tanapa Lugalo Open ni Miongoni mwa mashindano Makubwa
yanayodhaminiwa na Shirika la Hifadhi za Taifa TANAPA na kuvutia wachezaji
kutoka maeneo mbalimbali ndani na Nje ya Nchi.
No comments:
Post a Comment