Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na
Usafirishaji kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Mustafa Aboud Jumbe,
akizungumza jambo wakati akifunga kikao kazi cha mashirikiano kwenye Sekta ya
Ujenzi baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar, kilichofanyika kisiwani Pemba.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Maji, Nyumba na
Nishati kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Ali Khalil Mirza,
akishauri jambo wakati wa kikao kazi cha mashirikiano kwenye Sekta ya Ujenzi
baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi
Zanzibar, kilichofanyika kisiwani Pemba.
Wajumba kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, wakiwa katika kikao kazi cha
mashirikiano kwenye Sekta ya Ujenzi baina ya Serikali hizo, kilichofanyika
kisiwani Pemba.
Na Mwandishi Wetu
SERIKALI ya Tanzania na
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), zimesema zitaendelea kudumisha na
kuimarisha ushirikiano katika masuala mbalimbali ikiwemo miundombinu na
usafirishaji ili kukuza uchumi na maendeleo ya nchi.
Hayo yamesemwa na
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia Sekta
ya Ujenzi, Msanifu Majengo na Majenzi Elius Mwakalinga, wakati akifungua kikao
kazi cha mashirikiano kwenye sekta ya ujenzi, baina ya Serikali hizo
kilichofanyika Kisiwani Pemba Zanzibar
Mwakalinga, alisema
kuwa kupitia taarifa za utekelezaji ambazo
wakurugenzi wa taasisi wameagizwa kuziwasilisha kwao, zitawsaidia wao
kama watendaji wakuu kujua namna gani ya kutatua chagamoto hizo kwa pamoja ili
kufikia malengo waliojiwekea.
“Hatukuongea kipropaganda,
tumeongea kitaalaam namna ya kuboresha miundombinu na usafirishaji na tumepata
maoni kutoka kwa wajumbe namna ya kuondosha changamoto katika masuala haya kati
ya Serikali hizi”, alisema Katibu Mwakalinga.
Aidha, Mwakalinga, alifafanua
kuwa mkutano huo ni endelevu kwani nia na madhumuni yake ni kuhakikisha
wanajadili changamoto na kupata maoni ya wataalam kwa pamoja ambayo yatasaidia
katika kuboresha na kufanikisha maendeleo katika sekta ya ujenzi.
Kwa upande wake, Katibu
Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji kutoka Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar, Mustafa Aboud Jumbe, alisema lengo la kikao hicho ni
kubadilishana uzoefu.
Alisema kikao hicho kimeazimia
kwa kuwaagiza wakuu wa taasisi ambao ni wajumbe katika kikao hicho kuandaa
taarifa zao za utekelezaji na kuonesha changamoto zao ili kwa pamoja ziweze
kutafutiwa ufumbuzi.
Naye, Katibu Mkuu wa
Wizara ya Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati, Ali Khalil Mirza, alisema kuwa
kupitia vikao hivyo wataalamu kutoka pande hizo mbili watashauriana na
kubadilishana uzoefu ambao utasaidia kuboresha utendaji kazi katika maeneo ya
kazi.
Mkurugenzi kutoka
Kitengo cha Usalama na Mazingira, Mhandisi Julius Chambo, alisema Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar (SMZ), inashauriwa kuanzisha mizani katika barabara
zao ili kuzilinda na ziweze kudumu kwa muda mrefu pamoja na kuweka mifumo ya
kisasa ambayo itasaidia kupunguza mianya ya rushwa.
No comments:
Post a Comment