Na Irene Mark
MKURUGENZI
Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk. Agnes Kijazi
amesema mwaka huu mvua za masika zitaanza wiki ya pili ya Machi hadi
mwishoni mwa Mei mwaka huu, huku zikitarajiwa kuwa juu ya wastani.
Mvua hizo zitanyesha kwenye mikoa ya Kaskazini Mashariki ya nchi ambayo ni Manyara, Kilimanjaro na Arusha.
Dk.
Kijazi alisema hayo Dar es Salaam alipotangaza utabiri wa msimu wa
mvua za masika mbele ya waandishi wa habari na kuongeza kwamba mvua za
nje ya msimu zitaendelea hasa kwa maeneo ya Pwani ya Kaskazini yenye
mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani, visiwa vya Unguja na Pemba na
Kaskazini mwa Morogoro.
Kwa
mujibu wa taarifa za TMA mvua za masika mwaka huu zinafanana na
zilizonyeesha mwaka 2007 hivyo kuwataka wananchi kuchukua tahadhari ya
mafuriko na maafa mengine yatokanayo na mvua.
Alisema kutokana na mabadiliko ya tabia nchi, hali ya joto juu la wastani itaendelea kuwepo mpaka masika yatakapoanza.
"Maeneo
ya Pwani ya Kaskazini mikoa ya Dar es Salaam, ikijumuisha kisiwa cha
Mafia , Tanga na maeneo ya kaskazini mwa mkoa wa Morogoro pamoja
na visiwa vya Unguja na Pemba... ukanda wa Ziwa Victoria katika Mikoa
ya Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu na Mara pamoja na kaskazini
mwa mkoa wa Kigoma.
"Kutokana
na mifumo ya hali ya hewa ilivyo kwa sasa na inavyotarajiwa kuwa kwa
kipindi chote cha msimu huu kwa ujumla mvua za wastani zinatarajiwa
katika maeneo mengi ya nchi yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka.
"Hata
hivyo, maeneo mengi ya nyanda za juu Kaskazini Mashariki, Mashariki na
Kusini mwa Ziwa Viktoria, mkoa wa Tanga na visiwa vya Unguja na Pemba
yanatarajiwa kupata mvua za wastani hadi juu ya wastani kipindi cha
masika.
"...Upande
wa Magharibi mwa Ziwa Viktoria na maeneo mengine ya Pwani ya
Kaskazini mikoa ya Dar es Salaam na Pwani ikijumuisha kisiwa cha Mafia
na maeneo ya kaskazini mwa mkoa wa Morogoro yanatarajiwa kupata mvua za
wastani hadi chini ya wastani," alisema Dk. Kijazi
Kutokana
na hali hiyo ,TMA imewashauri wadau wa sekta mbalimbali ikiwemo Kilimo
na Usalama wa Chakula, Mifugo na Wanyamapori, Maliasili na Utalii,
Nishati na Maji, Miji, Afya na Menejimenti za Maafa kujipanga
kukabiliana na majanga.
Alisema
hali ya mafuriko inaweza kusababusha milipuko ya magonjwa na wadudu
waharibifu kujitokeza kutokana na unyevunyevu na kutuama kwa maji.
Mkurugenzi huyo alisema uwepo wa mvua za kutosha, utaongeza uzalishaji wa mazao mbalimbali na malisho ya mifugo na wanyamapori.
Alisema
mvua za Msimu zilizoanza Novemba, mwaka jana katika maeneo yanayopata
msimu mmoja wa mvua kwa mwaka, mikoa ya Dodoma, Singida, Tabora, Katavi,
Kigoma, Rukwa, Mbeya, Songwe, Njombe, Iringa, Ruvuma, Lindi, Mtwara na
Kusini mwa mkoa wa Morogoro zinaendelea vizuri kama ilivyotabiriwa.
"Tutaendelea
kutoa taarifa za mrejeo kila itakapowezekana hivyo tunaomba muieleze
jamii kwamba wazingatie zaidi tarifa za mrejeo zinazotoka kila saa24 na
vifurushi vya siku tano," alisisitiza Dk. Kijazi.
No comments:
Post a Comment