HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 11, 2020

WAKAZI WA KATA YA MISWAKI WILAYANI UYUI WAOMBA BWAWA LA MAJI YA KUTUMIA

Na Tiganya Vincent, TABORA

WAKAZI wa Kata ya Miswaki wilayani Uyui wameiomba Serikali kuangalia uwezekano wa kuwachimbia Bwawa la Maji ili kuwaondolea adha a matumizi ma maji ambayo sio salama na safi.

Kauli hiyo imetolewa jana na Diwani wa Kata Miswaki Antony Makani kwa niaba ya wakazi wa Kata yake alipokuwa akiwasilisha ombi kwa Wakala wa Maji safi na usafi wa mazingira Vijijini (RUWASA).

Alisema kutokana na umbali waliopo kutoka mradi wa bomba la Ziwa Victoria kuja Tabora hawatarajii kunufaika na maji hayo , njia pekee ya kuwasaidia ni kutumia mabonde yanayowazunguka kujengea mabwawa.

Makani alisema Kata hiyo ina wakazi zaidi ya 14,000 ambao wanalazimika kutumia maji ya madibwi ambayo yamechnganyikana na takataka mbalimbali ambazo zinaweza kuwasababishia magonjwa mbalimbali ya mlipuko.

Alisema eneo hilo liko katika ukanda wa Bonde la ufa ambao ni vigumu kupata maji kwa wingi kwa njia ya visima badala yake ni kwa njia ya kutega maji ya mvua.

Kwa upande wa Meneja wa RUWASA wilaya ya Uyui Meneja wa Wakala wa Maji safi na usafi wa mazingira Vijijini (RUWASA) Wilaya ya Uyui Godfrey Shibiti alisema kuwa ili Serikali ijenge bwawa lazima iangalie uwekezaji wa eneo husika ili kujiridhisha juu ya uwepo wa maji ya kutosha na kudumu kwa mradi.

No comments:

Post a Comment

Pages