HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 02, 2020

POLISI SINGIDA YAWATAKA WANANCHI KUPUUZA TAARIFA ZA WATU 14 KUUAWA WILAYANI MANYONI

 Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Singida, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ASP) Sweetbert Njewike, akizungumza na waandishi wa habari kukanusha kuwepo kwa mauaji wilayani Manyoni.
 Waandishi wa habari mjini hapa wakichukua taarifa hiyo.
Waandishi wa habari mjini hapa wakichukua taarifa hiyo.


Na Ismail Luhamba, Singida
  
JESHI la Polisi Mkoa wa Singida limewataka wananchi kupuuza habari zinazozagaa mitandaoni zinazodaiwa watu 14 wamekufa kwa kuchinjwa wilayani Manyoni.
Akizungumza na Waandishi wa habari mjini hapa, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Singida, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ASP) Sweetbert Njewike amesema taarifa iliyotolewa na  Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini , Godbless Lema ni ya uongo yenye lengo la kuleta taharuki kwa wananchi.
‘’ Lema alitoa taarifa hiyo wakati akitoa salamu kwenye msiba wa  Alex Jonas ambaye alikutwa  ameuwa kwa kukatwa  na kitu chenye ncha kali sehemu  mbalimbali za mwili wake katika eneo la Mbungani, ambapo alionyesha orodha ya watu 14 akidai waliuwa kwa kuchinjwa wilayani manyoni,bila ya kuwa na uhakika kama taarifa hizo ni sahihi, na kulituhumu jeshi la polisi mkoa wa Singida kuwa limeshindwa kutekeleza wajibu wake” alisema Njewike.
Aidha Njewike alisema kuwa matukio yote ya mauaji yaliyotolewa na Mbunge huyo yametokana na wizi,wivu wa mapenzi  na migogoro ya kifamilia na kuongeza kuwa wamefungua jalada la uchunguzi, dhidi ya mbunge huyo, uchunguzi  ukikamilika watachukua hatua za kisheria dhidi yake.

No comments:

Post a Comment

Pages