HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 17, 2020

Maalim Seif afurahiya maamuzi ya G20

Na Talib Ussi, Zanzibar
Chama cha ACT Wazalendo kimezitaka Benki ya Dunia na IMF kusimamia vyema nafuu ya madeni iliyotolewa na nchi za  G20 kwa nchi zinazoendelea kuhakikisha zinakuwa na mpango madhubuti wa kuigeuza nafuu hiyo kuwa fursa ya maendeleo ya watu na sio ya vitu.
Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa  chama hichoMaalim  Seif Sharif Hamad  Vuga Zanzibar baada ya kupata taarifa kuwa nchi zenye uchumi  mkubwa duniani ( G20)  zimekubali kusimamisha  malipo ya madeni ya nchi zinazoendelea ili ziweze kujipanga katika kupambana na Janga la maradhi ya Corona.
Alivitaka vyombo hivyo viwili kuhakikisha nchi zote ambazo zitapata nafuu hiyo lazima waonyesha  mpango unaotekelezeka wa kuimarisha sekta ya afya kwa upana wake.
“Lazima nchi hizo zionyesha mfumo wa uwajibikaji ili kuzuiya ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha” alieleza Mwenyekiti huyo.
Itakumbukwa Maalim Seif aliziomba nchi  za G20 kusimamisha madeni kwa nchi zinazoendelea ili zijipange vizuri katika kupambana na janga la maradhi ya korona hapo tarehe 4 april mwaka huu kupitia vyombo mbali mbali.
“Nimeupokea kwa furaha uwamuzi wa nchi zenye uchumi mkubwa duniani wa kusimamisha madeni yao kwa maslahi mapana ya kuwapa nafasi nchi hizo kupambana na janga hili lililotuingia Duniani kote” alieleza Maalim Seif.
Alisema uwamuzi huo ulichukuliwa juzi 15 April 2020na kufahamisha kuwa ni uwamuzi wa kihistoria unaojali maslahi mapana ya kihistoria.
Maalim Seif akitoa maombi hayo alifahamisha nchi hizo kuwa nchi kama Tanzania inatumia tsh trilioni 4 kila mwaka kulipia madeni  ya nje na Nchi za G20  jana zimeeleza zitastisha malipo ya madeni kuazia 1 may 2020 mpaka mwisho wa mwaka huu.
“Ni jambo la kushukuru sana kwani si haba, kwani itatusaidia sana  kukabiliana na athari za janga la korona” alieleza Maalim Seif.
Sambamba na hilo malim Seif akijinasibu kuwa chama chake ni chama pekee  kilichongoza katika juhudi za kuipata nafuu pia kitakuwa mstari wa mbele  kuhakikisha fedha hizo zinatumika kwa malengo yaliokusudiwa na kwamba zitakaguliwa na taasisi  huru ili kudhibiti mianya ya  matumizi mabaya.

No comments:

Post a Comment

Pages