HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 17, 2020

PUMA YAPULIZIA DAWA MAGARI KUUA VIRUSI VYA CORONA

 Mfanyakazi wa Kituo cha Mafuta cha Puma kilichoko mtaa wa Jamhuri jijini  Dar es salam akipulizia dawa baadhi ya magari yanayofika kituoni hapo kwa ajili ya kupambana na virusi vya Corona. (Picha na Denis Mlowe).



Na Denis Mlowe

KATIKA harakati za kupambana na virusi vya Corona nchini, kituo cha Mafuta cha Puma UMMA Mtaa wa Jamhuri jijini Dar es Salaam wameanzisha utaratibu wa kupuliza dawa za kuua vijidudu kwa wateja wote wanaokwenda kujaza mafuta katika kituo hicho.

Akizungumza na Habari Mseto Blog, Mkurugenzi wa Kituo hicho, Mohamed Ally, alisema kuwa utaratibu wa kupuliza dawa magari yanayofika katika vituo hivyo vya Mafuta kila siku.

Alisema mlipuko wa virusi vya corona ukiendelea kuathiri sekta zote duniani, mataifa mengi yameshindwa kupata jibu la kukabiliana na janga hivyo hakuna budi kuanza kupambana mapema visiendelee kuenea kwa kasi nchini.

Alipounga mkono kitendo cha agizo la kufungwa kwa shule na vyuo vyote nchini kubaki vile vile hadi hapo Serikali itakapotoa tamko jingine. 


Aidha alipongeza kitendo Cha serikali kuarisha maadhimisho ya Sherehe za Muungano, tarehe 26 Aprili 2020 pamoja na Sikukuu ya Wafanyakazi, Mei Mosi, 2020 ili kuepuka msongamano wa watu.

Mkurugenzi huyo alisema kuwa kitendo Cha Rais John Magufuli kusema watu wafunge na kusali ni jambo muhimu sana kwa sasa kwani kimbilio la kweli ni MUNGU.

No comments:

Post a Comment

Pages