HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 03, 2020

RC TABORA APOKEA MSAADA WA BARAKOO ZA SHILINGI MILIONI 20 KUTOKA KAMPUNI YA ATT

Ofisa usafirishaji wa Kampuni ya Usafirishaji (ATT)  Godfrey Tarimo(kushoto) akikabidhi jana msaada ya barakoa ya thamani ya milioni 20 kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri(kulia). (Picha na Tiganya Vincent).
 
 
 
Na Tiganya Vincent
 
KAMPUNI ya Usafirishaji ya Athwal (ATT) ya mjini Tabora imetoa msaada wa barakoo zenye thamani ya shilingi milioni 20  kwa uongozi wa Mkoa wa Tabora.

Msaada huo umekabidhiwa jana na Ofisa usafirishaji wa ATT Godfrey Tarimo kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora ili kuunga mkono juhudi za Serikali za kukabiliana na ugonjwa wa Covid-19.

Alisema Kampuni hiyo ambayo inatoa huduma za usafirishaji ndani na nje ya Tabora imeamua kutoa msaada huo ili uweze kusaidia katika mapambano dhidi ya virusi vya Corona yanayoendelea mkoani Tabora.

Akipokea msaada huo Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri, alisema msaada huo umekuja wakati muhimu ambapo Taifa liko katika vita ya kudhibiti ugonjwa wa Covid- 19 usiendelee kusambaa.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema wadau wote Mkoani humo wanapaswa kuungana katika vita ili hatimaye waweze kuushinda ugonjwa wa Covid-19.

Alisema msaada huo walioupokea baada ya kudhibitishwa na wataalamu wa sekta ya afya kuwa ziko vizuri zitagawanywa katika Wilaya zote za Mkoa wa Tabora kwa ajili ya kuwasaidia watoa huduma za afya ambao wanasaidia kukabiliana na ugonjwa wa Covid-19 na watu wengine ambao hajiwezi.

Mkuu huyo wa Mkoa alitoa wito kwa wadau wengine wanaoendesha shughuli zao ikiwemo za biashara kuendelea kushirikiana na Serikali katika mapambano dhidi ya janga la Corona.

No comments:

Post a Comment

Pages