HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 14, 2020

WATUMISHI WA UMMA WAMEONYWA MATUMIZI YA MITANDAO YA KIJAMII ISIYO RASMI KATIKA USAMBAZAJI WA NYARAKA ZA SERIKALI ZIKIWEMO BARUA ZA KIKAZI

Na Tiganya Vincent
 
WATUMISHI wa umma wameonywa kutotumia mitandao ya kijamii ambayo sio rasmi katika usambazaji wa nyaraka mbalimbali za umma zikiwemo barua za kikazi katika Ofisi nyingine za umma.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mkuu wa Kitengo cha  Sheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua Dustan Shimbo wakati akitoa mada kwenye mafunzo ya siku mbili ya awali kwa ajira mpya za Watendaji Kata, Watunza kumbukumbu, Makatibu Mahsusi, Madereva na Maafisa Tehama
Alisema ni marufuku kutumia barua za Kiserikali kwa kutumia mitandao kama ‘WhatsApp, facebook, na  e-mail’ binafsi kwa kuwa kufanya hivyo  ni kinyume na matakwa ya Sheria ya Usalama wa Taifa ya mwaka 1970.

Shimbo alisema kuwa Sheria hiyo imepiga marufuku wa utoaji wa nyaraka zote zilizohifadhiwa bila kufuata taratibu unaotakiwa na kuongeza unaweza kupelekea nyaraka hizo kuzagaa mitaani.

Alisema hatua hiyo inaweza kupelekea  jamii kupokea taarifa ambazo sio rasmi na ambazo hazikuwafanyiwa utafiti na hazikutoka Mamlaka inayopaswa kuzitoa , jambo ambali linaweza  kupelekea kuzuka kwa taharuki katika jamii na kuhatarisha usalama.

Shimbo alisema Mtumishi ambaye hakupewa Mamlaka ya Utoaji wa Taarifa akifanya kosa hilo atafungwa kwa kipindi cha miaka isiyozidi 20.

Alitoa wito kwa watumishi kuendelea kuzingatia taratibu zinazoruhusiwa kisheria katika usambazaji wa taarifa rasmi na kuachana na zile ambazo hazikubaliki ili kuwa na mazingira salama katika uendaji kazi wao.

Mmoja wa Watumishi wapya wa Halmashauri hiyo Scolastica Francis alisema kuna umuhimu sana kwa watumishi wa umma kutunza siri kwa sababu unasaidia katika kuimarisha umoja ndani ya utumishi wa umma.

Alisema utoaji wa siri unaweza kusababisha baadhi ya watumishi kuvamiwa kama wanapokuwa wamepata malipo yao stahiki.

No comments:

Post a Comment

Pages