HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 14, 2020

WAZAZI MKOANI TABORA WATAKIWA KUSHIRIKI UJENZI WA MADARASA KATIKA MAENEO YAO

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri (katikati) akikagua jana  mmoja ya chumba cha darasa katika Shule ya Sekondari Usinge iliyojengwa kwa kutumia tofali zilizofyatuliwa na wanafunzi kupitia mfumo wa elimu ya Kujitegemea wa Kaliua (Kaliua EK Model). (Picha na Tiganya Vincent).


NA TIGANYA VINCENT
 
WAZAZI Mkoani Tabora wametakiwa kutenga siku moja katika wiki ya kushiriki katika ujenzi wa miundombinu ya sekta ya elimu katika maeneo yao kwa ajili ya kuweka mazingira mazuri ya watoto kupata elimu.

Kauli hiyo ilitolewa jana wilayani Kaliua na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa miundombinu ya shule iliyojengwa kutokana na nguvu za wanafunzi ambayo itasaidia kupunguza uhaba wa vyumba vya madarasa.

Alisema muundo wa elimu ya kujitegemea unaotuumia Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua kwa kushirikisha jamii na wanafunzi katika ujenzi wa madarasa, maabara, mabweni na maktaba utasaidia kuboresha kiwango cha elimu kwa wanafunzi kwa kuwa na mazingira rafiki ya upataji elimu.

Mwanri aliipongeza Kaliua kwa uamuzi wake wa kutekeza wazo la Baba wa Taifa Mwalimu  Julius Kambarage Nyerere  kwa vitendo na kuagiza  kuwa Mkoa mzima ni lazima uanze kutumia wanaotumia Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua wa ujenzi wa vyumba vya madarasa na nyumba za walimu kwa kushirikisha wananfunzi na jamii ili  kupunguza uhaba wa miundombinu hiyo.
Aidha alisema Elimu ya kujitegemea ni lazima itiliwe mkazo ili iweze kuwaandaa wananfunzi kuwa tayari kujiegemea hata kama hakuendelea na masomo ya juu.

Akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua Dkt. John Pima alisema kupitia mfumo wa Elimu ya Kujiegemea ya Kaliua (Kaliua EK Model) wanafunzi wa shule za Msingi waweze kufyatua tofali zaidi  milioni 1.9 ambazo zimejenga vyumba vya madarasa 93, matundu ya vyoo 69 na nyumba za walimu 11.

Alisema kwa upande wa Shule za Sekondari wamefyatua na kuchoma tofali zaidi ya laki 6 ambazo zimesaidia kujenga vyumba vya madarasa 56 na matundu ya vyoo 36.

Dkt. Pima aliongeza katika kuunga mkono juhudi za wanafunzi na wananchi katika uekelezaji wa elimu ya kujitegemea ,Halmashauri hiyo imetoa  mabati bando 300 saruji mifuko 2,400 , mbao 2,072 kwa ajili ya ukamilishaji wa vyumba vya madarasa katika shule mbalimbali.

No comments:

Post a Comment

Pages