HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 27, 2021

MKUU WA MKOA WA PWANI AKUTANA NA WADAU WA ZAO LA KOROSHO WILAYANI RUFIJI KUJADILI NJIA ZA KUFANIKIWA

 

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Aboubakar Kunenge akizungmza katika kikao cha wadau wa zao la Ufuta kilichofanyika katika ukumbi wa Chuo cha ufundi stadi  cah (FDC) ambacho kilihudhuliwa na viongozi mbali mbali wa seriklai kwa lengo la kuweza kujadili mikakati ya kukza zao hilo.


Baadhi ya wadau wa zao la Korosho waliohudhulia katika kikao hicho ambacho kilikuwa na lengo la kujadili mambo mbali mbali juu ya suala hilo.

 

 

NA VICTOR MASANGU, RUFIJI

 

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Aboubakar Kunenge amekerwa na madhaifu mbali mbali yaliyopo kwa baadhi ya watendaji kutokuwa na tabia ya ucheleweshwaji wa Pembejeo za kilimo hali ambayo inawakwamisha wakulima kutoweza kufanya shuguli zao za kilimo kwa ufanisi ambao unatakiwa.

Kungenge ametoa kauli hiyo wakati akiendesha  kikao cha wadau mbali mbali wa zao la Ufuta kilichofanyika katika ukumbi wa cho cha ufundi stadi (FDC) Wilayani Rufiji amabpo kilihudhuliwa na wadau  mbali mbali wa maendeleo pamoja na viongozi wengine wa serikali wa ngazi za Wilaya na Mkoa.

 

Pia Mkuu   aliongeza kuwa anasikitishwa sana na kuona baadhi ya watendaji na viongozi wengine kuwa na urasimu na kuwataka wabadilike na kuhakikisha kwamba wanaweka mikakati madhubuti ambayo itawasaidi wakulima hao waweze kulima kilimo chao amabcho kina tija katika Mkoa wa Pwani.

“Kwa kweli  kwa upande wangu nina kerwa sana na madhaifu ambayo ambayo yanafanywa na baadhi ya watendaji wety, jambo hilo sio sawa kabisa hata kidogo na wengine bado wana tabia ya kufanya ursarimu lakini lengo letu sisi ni kuona wakuli wa zao la ufuta kwa kushirikiana na serikali wanalima killomo chenye tija.”alisema Kunenge.

 

Kadhalika aliwataka viongozi kuweka mpango kabambe ambao utaweza kuondokana na changamoto ya uhaba wa vifungashio vya ufuta na kwamba ataendelea kuwapa ushirikiano wa kutosha ili waweze kutimiza malengo yao waliyojiwekea.

Pia Kunenge aliongeza kuwa  katika kuwasaidia wakulima wa zao la ufuta kunaitajika ushirikiano madhubuti kutoka kwa wadau mbali mbali wa zao hilo ili kuweza kusimamia zoezi zima la uendeshaji wa  mnada wa kwanza  bila ya kuwa na ucheleweshwaji wowote.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa  aliwataaka wakulima  wote  kulima kilimo chenye Tija, na kuahidi kuwa serikali ya awamu ya sita ipo tayari  kuwasaidia ili waweze kuzalisha kwa kiwango kinachotakiwa na chenye kuleta mafanikio kwa Mkoa.

 

Kungene katika kikao hicho aliwaagiza Wataalamu mbali mbali wa kilimo pamoja na Ofisi yake  kufanya Tathmini ya zao hilo na kuja na Mkakati  endelevu ambao utaleta matokeo chanya katika sualazima la kukuza kilimo cha zao la ufuta katika Mkoa wa Pwani.

No comments:

Post a Comment

Pages