HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 14, 2021

RAIS WA ZANZIBAR ALHAJ DK.HUSSEIN ALI MWINYI ALIHUTUBIA BARA LA EID EL FITRY KATIKA UKUMBI WA SHEIKH IDRISA ABDULWAKIL KIKWAJUNI ZANZIBAR

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia Baraza la Eid El Fitry, lililofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu).

VIONGOZI wa meza kuu wakifuatilia hubata ya Baraza la Eid El Fitry wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akilihutubia katika ukumbi wa Sheikh.Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu).

MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi akiwa na Wake wa Viongozi na (kulia kwake) Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Zena Ahmed Said, wakifuatilia hutuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akilihutubia Baraza la Eid El Fitry, lililofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar. (Picha na Ikulu).

BALOZI Mdogo wa Oman aliyepo Zanzibar Mhe. Mohamed Ibrahim Al-Bulushi, akiwa na wageni waalikwa wakifuatilia hutuba ya Baraza la Eid El Fitry, wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi akihutubia katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu).

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi akizungumza na kuwasalimia baadhi ya Masheikh wa Zanzibar waliofika Ikulu kwa ajili ya kumsalimia baada ya kumalizika kwa Sala ya Eid El Fitry. iliofanyika katika viwanja vya Maisara Suleiman Jijini Zanzibar. (Picha na Ikulu).
 
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi akimpa Mkono wa Eid Bw. Mohammed Ali Mzee, katika viwanja vya Ikulu Jijini Zanzibar. (Picha na Ikulu).

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi akiwasalimia Wananchi waliofika katika viwanja vya Ikulu Jijini Zanzibar kwa ajili ya kumsalimia na kupokea mkono wa Eid El fitry. (Picha na Ikulu).

No comments:

Post a Comment

Pages