HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 21, 2021

TASAF yapewa Sh Bilioni 5.5 za Utekelezaji Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano ya UVIKO 19


Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko huo Ladislaus Mwamanga.

 


Na Hussein Ndubikile, Dar es Salaam
 

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania (TASAF) umetengewa Sh Biloni 5.5 zitakazoelekezwa katika utoaji wa ruzuku na utekelezaji wa Miradi ya Ajira za muda kwa kaya za walengwa ili zipate kipato  cha kuziwezesha kujikwamua kiuchumi na kupunguza athari za Uviko 19 pamoja na kuongeza rasilimali na miundombinu ambayo itatumika na jamii yote katika Mitaa na Shehia.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko huo Ladislaus Mwamanga wakati akitoa taarifa kwa wanahabari kuhusu Utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya Uvko 19 kwa Mpango wa kunusuru Kaya za Walengwa wa TASAF.

Amesema kuwa fedha hizo ziwafakikia kaya za walengwa 40,740 wenye uwezo wa kufanaya kazi amabao wanaishi katika maeneo ya mjini, watafanya kazi za miradi ya jamii na kulipwa ujira wa Sh 135,000 kwa kila kaya ili kufufua na kuimarisha shughuli zao na kukuza uchumi wa kaya zilizoathirika zaidi na ugonjwa huo.

" Mfuko umeidhinishiwa Sh Bilioni 5.5 kati ya fedha zilizotolewa kama mkopo wenye masharti nafuu kukoka Shirika la Fedha Kimataifa (IMF) itazitumia  fedha hizo kuondoa athari za kiuchumi zilizochewa wa Uviko 19  kwa kaya walengwa ambazo Serikali imedhamiria kuwaondoa katika umaskini wa kipato kwa kuwapatia ruzuku za kujikimu, ajira za muda , kuwaongezea ujuzi,  maarifa na elimu ya ujasiriamali ili wakidhi mahiaji yao," amesema Mwamanga.

Amebanisha kuwa Serikali inaendelea kutekeleza mpango na mikakati mbalimbali katika kupunguza umaskini wa watanzania wanaoishi katika mazingira duni na kwamba inafanya jitihada kubwa kupata vyanzo vya ndani, mikopo na misaada kutoka wadau wa maendeleo ili kuhakikisha watanzania wanaondokana na umaskini.

Amesisitiza kuwa muda wa matumizI wa fedha hizo umewekwa bayana na kwamba Menejimenti ya TASAF kwa mwongozo wa Kamati ya Uongozi ya Taifa itahakkisha maandalizi ya utekelezaji wa miradi ya ajira za muda kwa walengwa katika maeneo yatakayoanishwa utaanza mara baada ya fedha hizo kupokelewa.

Amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kusimamia vyema mapambano dhidi ya UVIKO 19 ambayo yamefanikisha kupata mkopo wenye masharti nafuu wa Dola za Kimarekani Milioni 567 sawa na Sh Trilioni 1.3 kutoka IMF kwa ajili ya Kampeni kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano ya Uviko huo.

Amemuhakikishia Rais Samia kwamba utekelezaji wa miradi utafanywa kwa wakati na hakuna fedha zitakazotumika nje ya malengo yaliyokusudiwa kwa walengwa wa TASAF.

Ameongeza kuwa  TASAF inatekeleza Mpango wa Kunusuru Kaya za walengwa katika Halmashauri za Tanzania Bara, Unguja na Pemba na kwamba idai yao ni takribani kaya milion 1.4 zenye watu wanaokadiriwa milioni 10 wanaotoka kaya zinazoishi katika mazingira duni.

No comments:

Post a Comment

Pages