- Asema ni utekelezaji wa maelekezo Rais Samia suluhu Hassan kuwalinda wafanyabiashara kutokana Na mabadiliko ya tabia nchi.
-
Asema Ujenzi unaanza rasmi wakati wowote kwa mawe kupangwa kuzuia
kumomonyoka kwa kingo Za bahari, kuweka paving na palms kupendezesha.
- Asema Coco Beach itakuwa sehemu Bora ya mapumziko kwa wananchi.
Mkuu
wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla leo amekabidhi kazi ya
Ujenzi wa Kingo za Kuzuia maji ya Bahari kwenda kwenye Vibanda vya
Wafanyabiashara eneo la Coco Beach ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya
Rais wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan aliyotoa juzi alipotembelea
ufukwe huo.
RC Makalla
amesema Mkandarasi huyo ataanza kazi ya kupanga mawe na kujenga Garden
ya kisasa ya Vigae kwenye eneo la mbele ya Vibanda ambalo kwa Sasa
limetawaliwa na vumbi.
Aidha
RC Makalla amesema Serikali imedhamiria kufanya ufukwe wa Coco kuwa
kimbilio la Wananchi kwaajili ya matembezi, mapumziko, chakula na
vinywaji.
No comments:
Post a Comment