Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania Bw. Macrice Mbodo (wa pili kulia) akiwa na Mkurugenzi Mkuu TANTRADE, Latifa Khamis (kulia) Mkurugenzi mkuu wa TTCL Mhandisi Peter Ulanga (kushoto), pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa UCSAF Bi. Justina Mashiba (wa pili kushoto) wakisubiri kumpokea Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Nnauye wakati wa hafla ya Siku ya Posta iliyofanyika katika viwanja vya Maonesho ya 46 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba), jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye, akizungumza wakati wa hafla ya Siku ya Posta iliyofanyika katika viwanja vya Maonesho ya 46 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba), jijini Dar es Salaam.
Na Mwandishi Wetu
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye, atoa wito kwa wananchi kuendelea kutumia huduma za Shirika la Posta kwani kwa sasa Shirika limeboresha huduma zake kuwa za kisasa kulingana na mahitaji ya wananchi.
Hayo ameyasema
jijini Dar es Salaam wakati alipohudhuria Siku maalum ya Shirika la
Posta katika viwanja vya Maonesho ya 46 Kimataifa ya Biashara
(Sabasaba), jijini Dar es Salaam
Aidha,
Waziri ametumia nafasi hiyo kulipongeza Shirika la Posta Tanzania kwa
juhudi inayoendelea kuzifanya katika kutoa huduma bora na stahiki
kulingana na mahitaji ya wananchi hususani katika kipindi hiki cha
maendelea ya TEHAMA
Sambamba
na hilo, Nape amepata fursa ya kutembelea mabanda mbalimbali viwanjani
hapo ikiwemo Banda la Shirika la Posta Tanzania na kujionea huduma
mbalimbali zinazotolewa katika viwanja hivyo
Naye,
Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania Macrice Mbodo ameelezea
huduma mbalimbali zinazotolewa na Shirika hilo viwanjani hapo ikiwemo
huduma za EMS, Duka Mtandao, Posta Kiganjani, Huduma za kubadilisha
fedha za kigeni na Uwakala ikiwemo ukataji wa tiketi za ndege ya ATCL
Pia,
Postamasta Mkuu ametumia nafasi hiyo kuendelea kuwakaribisha wananchi
katika banda la Posta lililopo viwanjani hapo ili kuendelea kufurahia
huduma za kisasa
Hafla
hiyo ya Siku maalum ya Posta imehudhuriwa Viongozi waandamizi na
wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania pamoja na wasanii mbalimbali wa
maigizo (Bongo Movie) ikiwemo Swebe, Snura, Tausi Mdegela, Dr Kumbuka,
Asha Boko, na wengine mbalimbali.
No comments:
Post a Comment