NA TATU MOHAMED
SERIKALI imeyapandisha hadhi maonesho ya dhahabu yanayofanyika mwezi Septemba ya kila mwaka mkoani Geita na kuwa ya kitaifa.
Kufuatia
kupanda hadhi kwa maonesho hayo Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara
Tanzania (Tantrade) wameingia makubaliano na mkoa wa Geita ya
kuhakikisha maonesho hayo ya dhahabu yanakuwa na hadhi hiyo ya kitaifa.
Akizungumza
wakati wa utiaji saini wa makubaliano hayo uliyofanyika katika
maonesho ya 46 ya biashara ya kimataifa, Mkuu wa Mkoa wa Geita Rosemary
Senyamule amesema makubaliano hayo yatakwenda kuyafanya maonesho hayo ya
dhahabu kuwa makubwa kuliko yote yanayofanyika hapa nchini.
Amesema
maonesho hayo ya dhahabu kuwa ya kitaifa yatasaidia kukua na kuwavutia
wawekezaji wengi ndani na nje ya nchi kushiriki katika kuonesha bidhaa
zao.
"Tunafahamu kuwa
muda uliobakia ni mchache kwani Septemba ndiyo yatafanyika maonesho ya
dhahabu mkoani Geita, tumeshawaambia wadau kuwa hatutayapeleka mbele
hivyo kwa kushirikiana na Tantrade tutakaa pamoja na kukubaliana namna
bora ya kuyaboresha ili yaonekane ya hadhi na kisasa," amesema
Naye
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Geita, Zahra Michuzi amesema makubaliano
hayo yatasaidia kuleta mapinduzi na kufanya mabadiliko kwenye teknolojia
ya dhahabu.ndani ya mkoa wa Geita.
Amesema
wanataka kufanya mageuzi makubwa katika sekta ya madini ya dhahabu
hivyo kupanda hadhi kwa maonesho hayo kutachagiza mabadiliko hayo.
"Tumepokea
kwa furaha nia njema ya kuingia makubaliano na Tantrade kwani kutafanga
maonesho hayo kutambulika nchini na kupanua wigo mpana wa ufanyaji
biashara," amesema
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Tantrade, Latifa Khamis amesema
kusainiwa kwa makubaliano hayo kutakwenda kuimarisha na kuufanya uwanja
wa Geita kuwa wa kisasa kwa ajili ya maonesho ya dhahabu.
No comments:
Post a Comment