HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 05, 2022

SMZ yajivunia mapato ya zaidi ya bilioni 3

 


Dk. Mngerza Miraji (kushoto) aliyekua katibu Mkuu Wizara Maji, Nishati na Madini na kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar akimkabidhi katibu Mkuu mpya wa Wizara hiyo, Joseph Kilangi, nyaraka za wizara hiyo baada kusaini fomu ya makabidhiano.

 

Na Talib Ussi, Zanzibar


Serikali ya Mapinduzi  Zanzibar  (SMZ) kupitia Wizara ya Maji, Nishati na Madini imeingiza mapato ya shilingi bilioni tatu na milioni hamsini na sita kwa kipindi cha miezi mitatu ikiwa ni mauzo ya maliasili zisizorejesheka ikiwemo kifusi, mchanga  mawe, kokoto na vumbi.

Hayo yameelezwa na aliyekuwa katibu mkuu wa wizaya hiyo Dkt Mngerza Mzee Miraji wakati akimkabidhi ofisi katibu mkuu mpya wa wizara  hiyo Joseph John Kilangi aliyekuwa katibu mkuu wa wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi.

Dkt. Mngereza amesema kutokana changamoto za upotevu wa maliasili kwa kushirikiana na watendaji wake waliamua kuchukua hatua za makusudi kuazisha mfumo wa kuombea maliasili zisizorejesheka ili kuzuia upotevu mali hizo. Hivyo April hadi June wizara hiyo imeweza kuingiza fedha hizo  ambapo  mwezi wa Juni pekee uliingiza shilingi bilioni moja na nusu.

“Mfumo huu ni mzuri sana kwani unaweza kuona gari inapoingia katika shimo la maliasili, mali iliyobeba, uwezo wa gari, na wapi inaelekea hali ya kuwa nipo ofisini hata usiku. Pia   mtu akilipa  malipo benki kupitia mfumo huu unaonesha fedha zilizoingia aina zote za malipo kuanzi kibali shilingi 3000, kutokana na kamera zilizofungwa. Hii ndio ilikuwa kazi ngumu ya kudhibiti upotevu wa maliasili” alisema Mngereza


Aidha Dkt. Mgereza aliwashukuru watendaji kazi wa wizara hiyo  kwa mashikiano makubwa waliyompa katika kipindi chote alichotumika wizara hiyo kwani walikuwa wakifanya kazi kwa mashikiano ya karibu hali ambayo imeonesha dhamira ya Serikali katika kuwaletea wananchi  wake maendelo.

Kwa Upande wake Katibu Mkuu wa Wizara Hiyo Joseph J. Kilangi aliyekabidhiwa amesema anaamini yote aliyokabidhiwa atayaendeleza kwa dhati ile ile  hivyo, amewaomba watendaji wa wizara hiyo kumpa mashirikina kama walivyompa Dkt Mngereza kwasababu wote wanajenga nyumba moja ya kutekeleza ahadi za Serikali ya awamu ya nane inayongoza na Dkt Hussein Mwinyi.

Aidha amewataka watendaji wa wizara hiyo kutomchoka mapema kutokana na kuwaita mara kwa mara kwani majukumu hayo ni mapya kwake hivyo anahitaji kujifunza mambo mengi kupitia kwao.  Amesema anaamini akipewa mashirikiano hakuna kitakacho mshinda kwani kinachohitajika ni uwazi na uwajibikaji.

Mapema Waziri wa wizara hiyo amemshukuru Dkt Mngereza kwa mashirikiano makubwa aliyompa pamoja na juhudi za kuanzisha mfumo huo. Amesema mashirikinao ya Dr Mngereza yameweza kufanikisha bajeti  ya wizara hiyo kupita kwa urahisi hivyo amewataka watendaji wa wizara hiyo, kuendeleza ili ufanisi upatikane.

Makabidhiano hayo yamekuja kufuatia uteuzi aliyoufanya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapiduzi Zanzibar Dkt Hussein  siku ya June 30,2022 wa kuwateua manaibu katibu mkuu pamoja kuwabadilisha makatibu wakuu wa wizara mbali mbali za SMZ.


 

No comments:

Post a Comment

Pages