HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 28, 2022

Jifunze njia za kufaidika na Uwekezaji, Bima kwa pamoja






NA MWANDISHI WETU 


BIMA ni njia ya ulinzi wa kiuchumi dhidi ya hasara ya kifedha au hata  dhidi ya kifo ambayo watu au kampuni wanafuata kwa kulipa kiasi fulani kwa shirika la bima kwa mkataba maalum. Kuna aina mbalimbali za bima kuna bima ya afya, bima ya nyumba, bima ya vyombo vya moto, bima ya maisha na bima ya ulemavu.


Bima ya afya


Bima ya afya humsaidia mwanachama aliekata bima hiyo kupata matibabu na dawa endapo atapata matatizo ya kiafya ama maradhi mbali mbali.

Bima ya nyumba


Bima ya nyumba humsaidia mkata bima endapo atapata matatizo ya huaribifu wa nyumba yake kama moto na athari zingine, basi shirika hilo la bima litamlipa ama kufidia hasara iliotokea na kama huaribifu ni mkubwa zaidi na kufanya nyumba hiyo kuteketea kabisa basi shirika hilo la bima litampatia nyumba nyingine.

Bima ya vyombo vya moto


Bima hii humsaidia mkata bima ama mwanachama kulipwa fidia endapo chombo chake kitapata matatizo ama huaribifu na aina ya vyombo hivyo vya moto ni magari, bajaji na piki piki. Endapo gari yako itapata huaribifu mkubwa sana na kushindwa kutengenezwa basi utalipwa pesa yenye thamani ya gari yako.

Bima ya maisha


Bima ya maisha ni aina ya bima ambayo huhusika zaidi na kuwalipa watu walio orodheshwa na mtu aliekata bima kama wanufaika pindi anapoaga dunia ama kufariki.

Bima ya ajali


Bima ya ajali humsaidia mwanachama kulipwa fidia endapo atapata matatizo yalio sababishwa na ajali mfano ulemavu wa kudumu na matatizo mengine.

Nini maana ya uwekezaji?


Uwekezaji ni nyongeza ya mali inayoingiza mapato. Mali hizi ni zile ambazo zina wigo wa kuthaminiwa zaidi, thamani yao huongezeka kwa muda na kuwa chanzo cha mapato kwa mwekezaji. Ama kwa lugha nyepesi uwekezaji ni namna ya kufanya fedha zako ziweze kuzaa fedha zingine.


Ili uweze kuwekeza una hitaji kuwa na chanzo cha mapato kama biashara ama ajira hata kama ni kidogo, fedha ama pesa unayoipata kwenye chanzo hicho basi unatenga kiasi kidogo na kuwekeza ama una weka akiba kidogo kidogo na badae ikifika kiwango fulani unawekeza.


Je! Vipi endapo utapata mfumo ambao utakupa nafasi ya kupata bima na uwekezaji kwa pamoja? basi UTT AMIS kupitia mfuko wake wa wekeza maisha ni jibu la swali hili.


UTT AMIS ni taasisi ya serikali inayofanya uwekezaji wa pamoja ilio chini ya wizara ya fedha na mipango. UTT AMIS ilianzishwa mwaka 2005 na imefanya na inaendelea kufanya kazi nzuri ya uwekezaji wa pamoja hadi sasa, na kwa kipindi chote icho kuanzia 2005 hadi sasa 2022 iliunda ama kuanzisha mifuko mbali mbali ya uwekezaji wa pamoja, moja ya mifuko hiyo ni wekeza maisha.

Uwekezaji wa pamoja ni nini?

Uwekezaji wa pamoja ni mfumo unao lenga kukuza mitaji ya wawekezaji na kutoa nafasi kwa mtu ama watu wenye nia ya kuwekeza hata kama wana kiwango kidogo cha pesa.


Mfuko wa wekeza maisha ulianzishwa mwaka 2008 kwa lengo la kukuza mitaji ya watanzania pamoja na kutoa bima.

 

 Mfuko huu tangu umeanzishwa umekua mara saba hii inamaanisha aliweka elfu kumi sasa ana elfu sabini, alieweka laki moja sasa ana laki saba, alieweka milioni moja sasa ana milioni saba, alieweka milioni mia sasa ana milioni mia saba nk. Mpaka sasa mfuko una thamani ya bilioni 5 za kitanzania. Mfuko wa wekeza maisha umetoa nafasi ya uwekezaji kwa Watanzania wenye umri wa miaka 18 hadi 55.

Mwekezaji anafaidikaje na mfuko wa wekeza maisha?

Ukiwekeza kwenye mfuko huu utapata faida ya kuongezeka kwa mtaji wako nikimaanisha pesa unayoiweka ama kuwekeza kwenye mfuko huu inaongezeka taratibu taratibu na kwa muda mrefu hutengeneza faida nzuri, na pia utapata bima.
Kuna bima za aina mbili kuna bima ya maisha pamoja na bima ya ajali ambayo itakusababishia matatizo kama ulemavu wa kudumu.


Mfuko huu una kiwango cha chini cha uwekezaji pamoja na ukomo wa faida za bima, kiwango cha chini cha uwekezaji ni shilingi milioni moja kwa kipindi chote cha uwekezaji, na unampa mwekezaji nafasi ya kuchagua mpango wa kuiweka pesa hiyo kidogo kidogo au kuiweka kwa mkupuo. Ukomo wa faida za bima kwenye mfuko huu ni shilingi milioni 25 kwa kipindi chote cha uwekezaji hii inamaanisha hautolipwa zaidi ya milioni 25 kama utapata matatizo.


Akipata ulemevu wa kudumu (kupoteza uwezo wakuona macho yote mawili, kupoteza mikono ama miguu yote miwili, kupoteza uwezo wa kusikia masikio yote mawili.) atalipwa fidia ya asilimia 100.


Mwekezaji akifariki mrithi wake au warithi wake aliowaorodhesha Bima itamlipa mwekezaji kuanzia asilimia 5 hadi 100 ya milioni 25 kulingana na tatizo husika. watalipwa pesa yote aliochangia na faida zilizo zalishwa na kama mwekezaji alifariki kabla ajamaliza uwekezaji wake ama kiwango alichosema atawekeza kwa kipindi chote cha uwekezaji basi kile kiwango ambacho hakufanikiwa kukimaliza ama kuwekeza mrithi au warithi wake watapewa, kwasababu taasisi ya UTT AMIS inaamini kua mwekezaji kama angepata nafasi yakuwekeza angeweza kumaliza kiwango chake cha uwekezaji kwa muda wote huo.  


Mfuko huu pia una gharama za mazishi ambazo ni 500,000 na pesa hii atapata mrithi ama warithi wa mwekezaji pale anapowasilisha kibali cha mazishi kwenye ofisi za UTT AMIS, na pesa hiyo italipwa kwa mrithi ama warithi walio orodheshwa na mwekezaji.


Pesa zitakazokua zinatoka kulipa fidia ya tatizo lililotokea ni pesa za bima na sio pesa za mwekezaji alizowekeza kwenye mfuko, asilimia 99 ya pesa ya mteja itawekezwa na asilimia 1 tu ndo itaenda kulipa gharama za bima.


Mfuko huu unamuda wa kuwekeza ama uwekezaji. Mwekezaji akiwekeza kwenye huu mfuko itambidi akae kwenye huu mfuko kwa kipindi cha miaka kumi. 


Unaweza kuona miaka kumi ni mingi ila kwa mtu mwenye malengo ya muda mrefu na mwenye nia ya uwekezaji basi kwake hatoona kama ni miaka mingi bali ataona fursa ya kupata nafasi ya kuwekeza kwa muda mrefu na kutengeneza faida nzuri zaidi.


Mwekezaji akimaliza kipindi chake chote cha uwekezaji atapata mkono wa pongezi kutoka UTT AMIS wa asilimia 5 na asilimia 7, mwekezaji atapata asilimia 5 endapo alikua anawekeza kidogo kidogo kufikia kiwango chake alichosema na mwekezaji atapata asilimia 7 kama aliweka pesa hiyo kwa mkupuo ama kuweka kiasi chote cha pesa kwa pamoja.


Naomba nikueleweshe vizuri asilimia tano na saba sio ya pesa uliowekeza tu kwa miaka kumi bali ni pesa yako uliowekeza na faida zilizotengenezwa kwa miaka yote kumi. Tunajumlisha pamoja na kupata kiwango kamili cha pesa zako kwa muda wote wa uwekezaji alafu tunakupa asilia tano au saba tena kama mkono wa pongezi kwa kutimiza malengo yako uliojiwekea miaka kumi nyuma.

No comments:

Post a Comment

Pages