HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 21, 2023

 Luteni Kanali Mshana afanya ziara , aahidi ushirikiano

Mkuu was kikosi Cha 06 akimkabidhi  Mkuu wa Mkoa wa BERIBERATI Mambele kadei fulana yenye nembo ya Mali ya asili kama moja ya kutanga za utaliinwa Tanzania (kushoto).



Mkuu wa Kikosi cha sita cha Walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania (TANBAT 6), Luteni Kanali Amani Stephene Mshana ametoa shukurani zake Kwa Mkuu wa Mkoa wa Beriberati  Mambele Kadei akieleza kuwa amefarijika kumtembelea huku akiahidi ushirikiano wa karibu katika jukumu la kulinda amani ya wananchi wa Afrika ya Kati.


Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Ofisa habari wa kikosi hicho, Kapteni Mwijage Inyoma alisema Luteni Kanali Mshana ameahidi kushirikiana na mkoa huo katika jukumu la kulinda amani ya wananchin wa Afrika ya kati pamoja na kuwapa taarifa pale ambapo kutahitajika msaada wa kusimamia amani Kwa wananchi wa Mambele.


Naye Mkuu wa Mkoa huo baada ya ziara hiyo alisema Kuwa,"Tanzania na wanajeshi wake wana upendo sana kwetu, sisi ni kama dada au kaka au mama na hata baba hivyo kuja kwako Mkuu wa Kikosi kunitembelea kama ziara yako kwangu  ni ishara tosha kwa undugu wetu namimi ninahaidi ushirikiano huu kudumisha kama ilivyokuwa kwa vikundi vilivyopita kutoka Tanzania,"


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya hiyo alisema tangu kikundi hicho kimefika, kimeonyesha kasi kubwa katika ushirikiano wa karibu na wananchi wake anaowaongoza hapo Mambele kadei.


"Tumeshudia mkitoa matibabu, dawa hata elimu za ujasiliamali kwa akina mama na vijana Ili wajipatie kipato na kuepuka kuingia katika vikundi vyenye nia mbaya na serikali, hii ni ishara tosha kwetu kuwa walinda amani kutoka Tanzania chini ya Umoja wa Mataifa wanafanyakazi kuwa yenye tija kwetu tangu waanze  jukumu la ulinzi wa amani"


No comments:

Post a Comment

Pages