HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 12, 2023

MADIWANI WILAYANI KYERWA WATAKIWA KUMALIZA KERO SUGU KATIKA MAENEO YAO

.


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilayani Kyerwa Daniel Damian akitoa maelekezo ya Serikali kwa viongozi wa Halmashauri hiyo.



Na Lydia Lugakila Kyerwa


Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa   Mkoani Kagera wameagizwa kuhakikisha wanatatua kero Sugu katika maeneo yao.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilayani Kyerwa Mkoani Kagera Daniel Damian katika Kikao Cha Baraza la Madiwani kilichofanyika  katika Ukumbi wa Halmashauri hiyo.

Daniel amesema kuwa Maagizo ya  Chama Cha Mapinduzi  yanaelekeza Madiwani kutimiza Majukumu yao katika kutatua kero Sugu  bila kujali itikadi za Chama fulani.

"Chama chochote cha Siasa kinatakiwa  kuhakikisha kinatekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi ambapo kila Diwani ahakikishe anashughulikia kero zote ili wananchi wasikwame katika shughuli za kimaendeo" alisema  Mwenyekiti huyo.

Amesema Chama Cha Mapinduzi hakitamuonea huruma Diwani yeyote atakayeonyesha dalili za uzembe katika eneo lake na kuwa atakayeshindwa kuwajibika katika utatuzi wa Kero Sugu atachukuliwa hatua kisheria.

Katika Hatua nyinginezo Mwenyekiti huyo ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa  kutoa semina kwa Wakulima waishio Vijijini ili kuwasaidia kupata Hati miliki  za Kimila zitakazomruhusu mtu yeyote kwenda popote  kukopeshwa katika Taasisi za kifedha na kuendeleza shughuli za kilimo chenye tija.

Aidha ameitaka Ruwasa Wilayani humo kupeleka maji katika Taasisi zote za Kiserikali hasa katika Shule za Sekondari kwa wanafunzi wanaolala shuleni ili kuwanusuru na adha hiyo.

Hata hivyo amempongeza Rais Dkt Samia namna alivyoipendelea Halmashauri hiyo katika Miradi mbali mbali ya Maendeleo.

No comments:

Post a Comment

Pages