HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 09, 2023

MBUNGE JONAS MBUNDA AKABIDHI MABATI 968 NA FEHA MILIONI 21.2 UJENZI WA MIRADI

Viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Mbinga Mji wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa fedha na mabati na MBUNGE wa Jimbo la Mbinga Mjini Jonas Mbunda, wa kwanza kulia ni Mwakilishi wa Mbunge Betram Kapinga.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mbinga Mji Kelvin Mapunda, wa kwanza kulia ni Katibu wa Mbunge Jonas Mbunda Dotto Ponera wakiwa na viongozi mbalimbali
 

NA STEPHANO MANGO, MBINGA 

 

MBUNGE wa Jimbo la Mbinga Mjini  Jonas Mbunda amefanya hafla fupi ya kukabidhi fedha taslimu na vifaa vilivyonunuliwa kwa fedha za mfuko wa Jimbo kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ambazo ni bati 968 zenye thamani ya Tsh 31,944,000 Milioni na fedha taslimu Tsh milioni 21,200,000/= kwa ajiri ya utekelezaji wa miradi mbalimbali

Akikabidhi vifaa na fedha hizo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mbinga Kelvin Mapunda kwaniaba ya  Mbunge wa Jimbo la Mbinga Mjini Jonas Mbunda  ambaye yupo kwenye shughuli za  vikao vya bunge mjini Dodoma.

Mapunda alieleza furaha yake kama Kiongozi wa Halmashauri kuona changamoto zinazowasilishwa na Waheshimiwa Madiwani pamoja na wananchi zikipatiwa ufumbuzi wa haraka na viongozi amboa wanawategemea kuwasemea katika ngazi za juu.

Mapunda alisema kuwa mchanganuo wa Bati 968 kuwa kwenye Kata ya Luwaita -Zahanati ya Kijiji cha Tukuzi Bati 250, Kata ya Mbangamao -Ukimo shule ya Msingi Bati 140 , Zahanati ya Mikorola  Bati 26 Kata ya Luhuwiko- Ofisi ya Mtaa Luhuwiko Bati 120, Kata ya Matarawe - Ofisi ya Mtaa Puguru 150, Kipika shule ya msingi Bati 30

Alifafanua kuwa  Kata ya Bethrehem - Ofisi ya Kata Bati 120, Kata ya Mpepai - Luhangai S/M Bati 140 na kwamba jumla ya Bati  hizo 968 Bei ya bati moja ni Tsh 33,000/= kwa gharama ya Bati 968= Tsh 31,944,000/=

Alieleza zaidi kuwa mchanganuo wa Fedha Taslimu,Kata ya Mateka - Ukarabati Tanga shule ya msingi 5,000,000, Kata ya Myangayanga - Kitunda S/M Renta 2,000,000/=, Kata ya Kilimani - Ukamilishaji Zahanati ya Nzopai Tsh 4,000,000/=Kata ya Kihungu- Zahanati Mloweka Renta 2,000,000/=

Alisema kuwa Kata ya Kitanda- Ofisi ya Kijiji Renta 1,5000,000/=Kata ya Kikolo - Nyumba ya mganga Renta 3,500,000/= Kata ya Mpepai- Mpepai S/M Renta 2,000,000/= Kata ya Luhuwiko- Ukarabati wa Ofisi 1,200,000/=.ambapo jumla ya fedha Taslimu Tsh 21,200,000/=.

Aidha alimpongeza Mbunge kwa kujitoa kwake kutembelea Kata na Vijiji/mitaa kwenda kusikiliza changamoto zao na kutafuta namna bora ya kutatua.

 Alisisitiza Viongozi wa Kata na Vijiji /mitaa kusimamia vizuri fedha na vifaa vilivyotolewa ili ndani ya siku 21wananchi waone matokeo ya fedha na vifaa hivyo.

Naye, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Mbinga Enock Ndunguru alimpongeza  Mbunge kwa matumizi sahihi ya fedha ya mfuko wa Jimbo jambo ambalo linachochea maendeleo ya wananchi kama ambavyo mfuko huo umekusudiwa.

Ndunguru pia aliwataka wananchi kumshukuru na kuendelea kumpa ushirikiano mkubwa Mbunge kwani anaonyesha bidii kubwa ya kutatua changamoto zao.

Naye Katibu wa Mbunge Simoni Ponera akiongea kwaniaba ya Mbunge alimpongeza  Rais kwa kuongeza fedha ya mfuko wa Jimbo la Mbinga Mjini kutoka Milioni 34 hadi Milioni 58 kwani ongezeko hilo linampa Mbunge wigo mpana wa kutekeleza miradi mingi zaidi kuliko ilivyokuwa mwanzo.

Aidha, Alimshukuru  Rais kwa kutoa fedha zinazotekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ya Vituo vya Afya, elimu , maji ,Umeme n.k. pia alishukuru kwa ushirikiano mkubwa ambao Mbunge anaoupata kutoka kwa Viongozi wa Chama na Serikali ngazi ya Wilaya, Kata na Vijiji/Mitaa jambo linalorahisisha utekelezaji wa majukumu yake.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Mbinga Joseph Mdaka alisema kuwa Mbunge ameonyesha  uwazi  katika matumizi  ya mfuko  wa  jimbo na kwamba  ni  funzo  kwa wabunge wengine  wawe  wa  wazi  katika fedha na matumizi yake  yawe ya  kuchochea  shughuli  za  maendeleo  ya  wananchi  na  kugusa  mahitaji  sahihi ya walio wengi

No comments:

Post a Comment

Pages