HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 23, 2023

Mfumo wa kieletroniki (eGA) umesaidia kudhibiti upotevu wa mapato

Na Jasmine Shamwepu, Dodoma


MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Serikali mtandao Mhandisi Benedict Ndomba amesema mfumo wa kielektroniki wa eGA tangu kuanzishwa umesaidia kwa kiasi kikubwa kudhibiti upotevu wa mapato.



Mhandisi Ndomba, ameyasema  hayo leo jijini Dodoma wakati   akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu utekelezaji wa shughuli mbalimbali za Mamlaka hiyo ambapo amesema tangu kuanzishwa kwa mfumo huo umesaidia kudhibiti mianya ya ukwepaji wa malipo mbalimbali ya Serikali.


"Mfumo  wa ukusanyaji wa Malipo ya Serikali Kielektroniki (GePG) ambao umetengenezwa na Mamlaka kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha na Mipango, mfumo huu unaimarisha uwazi na udhibiti katika ukusanyaji mapato ya Serikali,”amesema Ndomba

 

Aidha Mhandisi Ndomba amebainisha maeneo sita ya kipaumbele kwa mwaka wa fedha  2022/2023 ambapo amesema kama mamlaka itaendelea kusimamia  sheria kanuni viwango na miongozo ya Serikali.


Aidha amesema Mamlaka itaandaa uwezo wa kutumia teknolojia mpya zinazoibuka, hasa zile za akili bandia, sarafu za kidijiti na teknolojia za kifedha, ili kuwezesha maboresho ya kiutendaji katika Taasisi za Umma na utoaji wa huduma kwa umma. 


MAMLAKA ya Serikali Mtandao ni Taasisi ya Umma ya   utoaji wa huduma kwa wananchi yenye  Lengo la kuongeza ufanisi wa utendaji kazi katika Taasisi za Umma pamoja na kuboresha utoaji wa huduma kwa Umma ili huduma hizo zipatikane kwa urahisi, haraka na kwa gharama nafuuk upitia TEHAMA.

No comments:

Post a Comment

Pages