HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 09, 2023

TTCL YASAINI MAKUBALIANO KUIHUDUMIA DRC KUPITIA MKONGO WA TAIFA

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Peter Ulanga (wa tatu kulia) pamoja na Mjumbe kutoka Shirika la Posta na Mawasiliano la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Bw. Ethiere Nkie Papy (wa pili kushoto) wakionesha nyaraka ya makubaliano ya ushirikiano kibiashara kati ya pande hizo mbili mara baada ya kusaini.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Peter Ulanga (kulia) pamoja na Mjumbe kutoka Shirika la Posta na Mawasiliano la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Bw. Ethiere Nkie Papy (kushoto) wakisaini nyaraka za makubaliano ya ushirikiano kibiashara kati ya pande hizo mbili Makao Makuu ya TTCL jijini Dar es Salaam.


Mshauri Mkuu wa Waziri, Wizara ya Posta na Mawasiliano na TEHAMA (DRC), Bw. Azitemina Fundji Blaise (aliyesimama) akizungumza kabla ya kusaini mikataba ya makubaliano ya ushirikiano kibiashara kati ya TTCL na Shirika la Posta na Mawasiliano la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Peter Ulanga (wa pili kulia) akizungumza kabla ya kusaini mikataba ya makubaliano ushirikiano kibiashara kati ya TTCL na Shirika la Posta na Mawasiliano la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Peter Ulanga (kulia) pamoja na Mjumbe kutoka Shirika la Posta na Mawasiliano la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Bw. Ethiere Nkie Papy (kushoto) wakisaini nyaraka za makubaliano ya ushirikiano kibiashara kati ya pande hizo mbili Makao Makuu ya TTCL jijini Dar es Salaam.


Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Peter Ulanga (kulia) pamoja na Mjumbe kutoka Shirika la Posta na Mawasiliano la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Bw. Ethiere Nkie Papy (kushoto) wakibadilishana nyaraka za makubaliano ya ushirikiano kibiashara kati ya pande hizo mbili mara baada ya kusainiwa katika hafla iliyofanyika Makuu ya TTCL jijini Dar es Salaam.

Picha ya pamoja kati ya wajumbe kutoka Shirika la Posta na Mawasiliano la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), wakiongozwa na Bw. Peter Ulanga Mkurugenzi Mkuu wa TTCL mara baada ya hafla ya makubaliano.   

 

SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limesaini makubaliano ya ushirikiano kibiashara na Shirika la Posta na Mawasiliano la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ikiwa ni pamoja na kunganisha Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kutoka Kigoma, Tanzania kwenda hadi Kalame, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

 

Hafla hiyo ya makubaliano imefanyika leo jijini Dar es Salaam kati ya viongozi wakuu wa mashirika ya pande zote mbili Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Tanzania, ikiwa ni kuendeleza ufanisi kiuchumi na kibiashara wa miundombinu ya Taifa ya Mawasiliano.

 

Akizungumza katika hafla hiyo ya kutiliana saini ya makubaliano, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Peter Ulanga amesema shirika hilo limeingia makubaliano ya kushirikiana na Shirika la Posta na Mawasiliano la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo katika mradi wa kunganisha Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kutoka Kigoma nchini Tanzania kwenda Kalame, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ikiwa ni umbali wa kilometa 150-160 kupitia Ziwa Tanganyika. 

 

"...Kutokana na ukubwa wa mradi huu, Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo leo hii tunasaini mkataba wa makubaliano ili kushirikiana katika kukamilisha mradi huu kwa ufanisi. Mradi huu ni muhimu sana kwa nchi zetu kwani utafungua njia za mawasiliano kati ya Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo pamoja na nchi jirani kama Kenya, Uganda, Malawi, Msumbiji na nje ya Bara la Afrika. Pia mradi huu utaiwezesha Tanzania kifika nchi za Pwani ya Magharibi kupitia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo," alisema Bw. Ulanga.

 

"Nichukue fursa hii kuwahakikishia Shirika la Posta na Mwasiliano la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuwa, Tanzania ni moja kati ya nchi mbili Afrika zenye uwezo wa kuunganisha Bahari ya Hindi na Bahari ya Atlantiki kwa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano. Pia tunayo miundombinu madhubuti ya mawasiliano na Serikali makini na wezeshi hivyo ni matarajio yetu kuwa mradi huu utafanikiwa," aliongeza Bw. Ulanga.

 

Aidha aliishukuru Serikali ya Tanzania chini ya Rais Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan na Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari chini ya Mhe. Nape Moses Nnauye kwa miongozo na ushirikiano wa dhati maouonesha kwetu Shirika la Mawasiliano Tanzania TTCL.

 

Pamoja na hayo, Bw. Ulanga amelishukuru Shirika la Posta na Mawasiliano la Jamhuri ya Demokrasia ya kongo na wawakilishi wa Shirika kwa kufikia hatua ya kusaini mkataba wa makubaliano kwa ajili ya kukamilisha mradi huo mkubwa wa kujenga miundombinu ya mawasiliano kwa maslahi mapana ya nchi zote mbili. 

No comments:

Post a Comment

Pages