HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 03, 2023

Wamiliki wa Shule wakumbushwa kutoingiza vitabu vyenye maudhui yasiyofaa

Wizara ya Elimu imewakumbusha wamiliki wa Shule kutoingiza shuleni  vitabu  vyenye maudhui ambayo hayaendani na mila na desturi na utamaduni wa nchi yetu.

Vitabu hivyo vimekuwa na hadithi ambazo maudhui yake yanahatarisha ukuaji na malezi ya mwanafunzi na pia kupotosha mila zetu katika makuuzi ya watoto na watanzania kwa ujumla.


Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dodoma  Katibu Mkuu wa  Wizara hiyo Dkt. Francis  Michael amesema hatua hiyo imefikiwa baada  ya kubaini kuwa kuna baadhi ya shule ambazo zimekuwa zikiingiza na kutumia vitabu ambavyo maudhui yake yanakinzana  maadili ya kitanzania.

Amesema ni vizuri wamiliki na waendeshaji wa shule wakafuata Waraka Na 4 wa mwaka 2014 uliotolewa na Wizara ambao pamoja na mambo mengine ulilenga kuhakikisha kuwa vitabu vya ziada na kiada vinavyotumika katika shule vina maudhui yanayoendana na mila na desturi na utamaduni wa nchi yetu.

"Wamiliki na waendeshaji wa shule zote za Umma na binafsi zilizosajiliwa hakikisheni mnafuata naa kuzingatia waraka  huo pamoja na miongozo inayosimamia elimu ili kuepuka kuchukuliwa hatua za kisheria na mpaka kufutiwa usajili shule," amesema Katibu Mkuu Michael

Amesema Wizara itaendelea kutekeleza wajibu wake wa kusimamia utoaji wa elimu na kuhakikisha njia za ufundishaji na ujifunzaji  zinazingatia  ubora na maslahi ya nchi.

No comments:

Post a Comment

Pages