HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 04, 2023

CCM yampa tano Mbunge koka kwa kupigania chachu ya maendeleo

 Na Victor Masangu, Kibaha 


Baadhi ya wanachama na viongozi wa chama Cha mapinduzi (CCM) kata ya Misugusugu wamempongeza kwa dhati Mbunge wa Jimbo la Kibaha mji kwa kutumia fedha za mfuko wa jimbo katika kuchagiza na kuchochea naendelea katika sekta mbali mbali.

Wanachama hao waliyasema hayo wakati wa ziara ya kamati ya siasa ya chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mji ambapo wamesema juhudi ambazo anazifanya zimeweza kusaidia kutatua baadhi ya kero na changamoto zilizopo.
 

Diwani wa kata ya Misugusugu Upendo Ngonyani wakati wa kusoma taarifa yake ya utekelezaji amesema kumefanyika mabadiliko makubwa katika sekta ya elimu kuboresha madarasa ambayo yamesaidia kupunguza msongamano kwa wanafunzi kazi ambayo imefanywa na Mbunge.

Kwa Upande wake Mbunge  wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka amesema ataendelea kushirikiana na wananchi katika kuwaletea maendeleo.

Pia aliongeza atahakikisha kwamba anaweka mikakati kabambe kwa ajili ya kupeleka uchumi katika maeneo mbali mbali ili kuweza kuwapa fursa wananchi waweze kupata huduma muhimu.

"Mimi nawaomba wananchi wa kata ya misugusugu ni vizuri kuweka mipango ya pamoja na kushirikiana na wananchi katika kuwaletea uchumi pamoja na kusimamia miradi mingine ya maendeleo,"alisema Koka.

"Tunataka tutengeneze mtandao wa Kuhakikisha kwamba watu wa Tarura au Tanrods ni lazima kwenda kwa wahusika ili kuweza kujua jinsi ya kutekeleza miradi yao ya maendeleo kwa kushirikiana kwa pamoja,"aliongeza Koka.

Kadhalika Mbunge huyo aliongeza anaendelea na juhudi katika kuboresha huduma ya maji safi na salama katika maeneo mbali mbali kwa wananchi wa kata ya misugusugu na maeneo ya viwanda na biashara.

Pia alisema ataendelea kutekeleza ilani ya chama Cha mapinduzi kwa vitendo na kusimamia fursa za ajira kwa vijana na kwamba lengo ni kuwakomboa wananchi kiuchumi na kupata ustawi kwa pamoja.

Katika hatua nyingine ameahidi kukivalia njuga baadhi ya watu ambao wanakabiliana na changamoto ya kunyanyaswa na wenye viwanda ambao wanafanya dhuruma kwa wafanyakazi wao.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) Wiaya ya Kibaha mji  Mwajuma Nyamka amekemea vikali  vitendo vya baadhi ya wanachama kuwa na makundi kwa ajili ya kupanga safu ya viongozi kabla ya uchaguzi kufika kwani ni kinyume kabisa na utaratibu.

Pia Nyamka aliongeza kuwa viongozi wa mashina wanapaswa kubadilika na kuweka mipango ya kuongeza idadi ya wanachama ili kuweza kukiimarisha chama pamoja na Jumuiya zake.

Ziara ya kamati ya siasa ya chama Cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mji imefanya ziara katika kata ya misugusugu kwa lengo la kuzungumza na wanachama pamoja na kutembelea viongozi wa ngazi mbali mbali.


No comments:

Post a Comment

Pages