HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 07, 2023

IET, ACRT na ERB kuadhimisha Siku ya Uhandisi Duniani kwa Maendeleo Endelevu, yawakaribisha Watanzania kushiriki

Na Hussein Ndubikile, Dar es Salaam


Taasisi ya Wahandisi Tanzania (IET) kwa kushirikiana na Chama cha Wahandisi Washauri Tanzania (ACRT) na Bodi ya Usajili ya Wahandisi Tanzania (EAFEO) ikiungana na Taasisi zote za Uhansisi Duniani kupitia Shirikisho la Taasisi za Kihandisi la Afrika Mashariki (EAFEO) na Shirikisho la Taasisi za Kihandisi la Afrika (FAEO) inatarajia kuadhimisha Siku ya  Uhandisi Duniani kwa Maendeleo Endelevu.

Akizungumza na Wanahabari Jijini Dar es salaam rais wa Taasisi hiyo Mhandisi Dkt. Gemma Modu amesema Maadhimisho hayo yatafanyika Machi 4 Mwaka huu katika Ukumbi Karimjee jijini humo yakiwa yamebeba ujumbe wa "Ubunifu wa Uhandisi kwa unaostahili zaidi " hiyo ni Kwa kuzingatia kuwa Dunia ipo zama za utandawazi ya Karne ya 21 na utashi kwenye Uchumi na Jamii zinazoendeshwa kwa nguvu ya Teknolojia ambayo maendeleo yake ni makubwa na ya kasi .

Amebainisha kuwa maadhimisho hayo ni fursa ya kuhamasisha  na kuhimiza vijana  wa kike na kiume ambao ndio taifa la kesho kuingia kwenye uhandisi ili kuhakikisha utekelezaji wa endelevu wa malengo ya maendeleo endelevu kwa miaka mingi ya mbele na vizazi vijavyo.

"Madhumuni ya siku hii  ni kutoa fursa ya kutambua na kuthamini mchango wa Uhandisi na watekelezaji wa kazi za Kiuhandisi wakiwamo Wahandisi na Mafundi wote katika kuleta Maendeleo endelevu ya Taifa letu kwa ujumla na kuboresha uelewa wa Umma kuhusu jinsi uhandisi wa Teknolojia ilivyo na umuhimu Kwa maisha yetu ya kila siku katika ulimwengu wetu wa Sasa"amesema rais Gemma

Gemma amewasisitiza Wahandisi Mapinduzi ya kidigitali yanaandamana na ubunifu wa sayansi huku matumizi yake lazima yalete tija katika uzalishaji wa bidhaa,utoaji huduma na uendeeshaji  wa Mifumo na utekelezaji wa  mikakati mbalimbali ya kukuza Uchumi kwa Maendeleo Endelevu kwani hayategemei tu ujuzi ..

Ameongeza kuwa maadhimisho hayo yanatarajiwa kuhudhuriwa na Washiriki zaidi ya 200 kutoka taasisi mbalimbali za umma na binafsi ambapo zitapata fursa ya kuonyesha bunifu zao katika kutekeleza miradi ya kimkakati inayoendelea nchini  huku wanafunzi wa vyuo na Sekondari watashiriki na kuonesha bunifu zao za masomo yao.

Amewakaribisha watanzania wote kujitokeza kwa wingi kwenye maadhimisho hayo kwani siku hiyo ni muhimu duniani katika sekta ya uhandisi ulimwenguni na umma kujua nini wahandisi na mafundi wanafanya kwa maendeleo endelevu.


No comments:

Post a Comment

Pages