HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 31, 2023

ZBA, TBA watembelea miradi ya kimaendeleo

Mkurugenzi wa Wakala wa Majengo Zanzibar (ZBA), Mhandisi Kassim Ali Omar (katikati) akiwa na watendaji wengine katika ziara ya kutembelea miradi ya kimaendeleo yainayosimamiwa na ZBA.



 Na Sabiha Keis (WAMM)


MKURUGENZI Mkuu Wakala wa Majengo Mhandisi Kassim Ali Omar amesema kuwa mashirikiano ya kiutendaji baina ya Wakala wa Mjengo Zanzibar(ZBA) na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) utaziwezesha Taasisi hizo mbili kuweza kufanya kazi kwa ufanisi zaidi kwa vile  majukumu yake yanalingana.

 

 Ameyasema hayo huko Jumbi  Wilaya ya Magharib “B”mara baada ya kumaliza ziara ya kutembelea miradi mbalimbali ya kimaendeleo ambayo Wakala wa Majengo Zanzibar ndio wasimamizi wakuu na washauri elekezi katika miradi hiyo.


Alifahamisha kuwa ziara hiyo ya watendaji kutoka Wakala wa Majengo Tanzania ni moja ya maagizo ya viongozi wa  nchi kuzitaka taasisi zinazofanana majukumu yake kushirikiana pamoja kiutendaji ambapo kwa sasa Taasisi hizo mbili zina mpango wa kutengeneza hati ya makubaliano(Mou)baina yao.


“ziara hii inalenga zaidi mashirikiano ya kiutendaji kwa taasisi mbili hizi na tayari tumeshafanya kikao ili tuweze kutengeneza hati ya makubaliano na tuweze kufanyakazi kwa karibu sana”alisisitiza Mkurugenzi huyo.


Kwa upande wake Mkurugenzi Wakala wa Majengo Tanzania(TBA) Mhandisi Loishorwa Likimaitare ameipongeza Taasisi ya Wakala wa Majengo(ZBA)kwa namna wanavojitahidi katika kutekeleza kazi zake za usimamizi wa miradi  ingawa  kumekuwa na uhaba wa watendaji kulingana na wingi wa kazi zilizopo hivyo ameiomba  Serikali kuwaongezea watenadaji hao ili waweze kufanyakazi kwa ubora na kukamilisha miradi wanayosimamia kwa wakati.


Tumefarijika sana kuja kuona kazi ambazo zinatekelezwa na wenzetu hawa na tumejifunza mengi kutoka kwao na hatua ya miradi wanayoisimamia kwa kweli inaridhisha hivyo nawaomba waongeze kasi ya uajibikaji ili Serikali iweze kuendelea kuwaamini”alisema Mkurugenzi huyo.


Nae Mhandisi Mohammed Nahoda Mohammed kutoka Wakala wa Majengo Zanzabar amefahamisha kuwa kwa Wakala inetekeleza miradi mbali mbali ikiwemo miradi ya ofisi ya uhamiaji ya Mkoa wa Mjini Magharib , mradi wa Shirika la Nyumba kwamchina na masoko matatu ya Chuini pamoja na Jumbi.


Aidha ameziomba taasisi mbali mbali za Serikali kuwatumia wakala wa majengo kwa vile taasisi hiyo ndio ipo kisheria na imepewa dhamana ya usimamizi wa miradi mingi ikiwemo ya Serikali na wamekuwa wakifanyakazi kwa kwa kiwango kinachokubalika nchini.


Akizungumzia kuhisiana na Ziara hiyo Mhandisi Daniel Mwakasungula kutoka Wakala wa Majengo Tanzania amefahamisha kuwa ziara hiyo ni miongoni mwa maagizo ya viongozi wa nchi kutaka Taasisi zinazolingana kimajukumu kuweza kushrikiana pamoja ili kuweza kupiga hatua za kimaendeleo nchini.


Miradi iliyotembelewa ni pamoja ofisi ya jeshi la uhamiaji mazizini,jengo la wakala wa chakula dawa na vipodozi,mradi wa ujenzi wa nyumba kwamchina,mradi wa soko la Mwanakwerekwe pamoja na Soko la Jumbi.


 

No comments:

Post a Comment

Pages