HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 25, 2023

DC Mpogolo awakumbusha Madereva Bodaboda kutii Sheria za Usalama Barabarani

Na Hussein Ndubikile, Dar es Salaam

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Edward Mpogolo amewataka Madereva Pikipiki (Bodaboda) kufanya shughuli zao za usafirishaji kwa kuzingatia taratibu na sheria za usalama barabarani ili kuepukana na madhara yanayoweza kujitokeza.
DC Mpogolo ameeleza  jijini Dar es Salaam wakati akizungumza Kwa Niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam katika mkutano uliowakutanisha madereva bodaboda kutoka maeneo mbalimbali nchi katika uzinduzi wa mfumo tambuzi wa data base wenye lengo la kuwasajili madereva hao kutambuliwa kwa haraka katika maeneo yao.

Amebainisha kuwa ni vyema wakabadilika sambamba na kufata taratibu za usalama barabarani Ili waweze kuepukana na changamoto ya kuchukuliwa hatua za mara Kwa mara kutokana na kukiuka sheria.

"Mhe Rais anawathamini na kutambua kazi munazozifanya kwani watu wengi wanapata ajira kwa kuuza pikipiki kwa wingi lakini pia mama Lishe kuwahudumia katika kuwapatia chakula"amesema Mpogolo

Amesema kuwa wanazipata riziki Kwa kuwa wanafanya shughuli za usafirishaji kutoka kituo kimoja mpaka cha pili hivyo jukumu lao kama wanataka amani nivyema wakabadilika.

Aidha amesema kuwa jiji la Dar es salaam limedhamiria kuweka vituo vya bodaboda katika maeneo ya jiji hilo ili waweze kutambulika kwa urahisi jambo ambalo pia litasaidia kuongeza mapato.

Awali akielezea Mfumo wa Utambuzi wa waendesha pikipiki Mratibu wa Mfumo wa Utambuzi UCC Elisha Masasi amesema kuwa malengo yao ni kuondoa na kuwadhibiti vishandu ambao wamekuwa wakifanya Madereva kuonekana hawafai Kwenye Jamii.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Madereva Bodaboda na Bajaj Dar es Salaam( SHIVYAMAPIDA), Michael Liganga amemuomba DC Mpogolo kuwaongezea idadi ya vituo madereva bodaboda na kuwatatulia chanagamoto ya kupata vitambulisho ili waweze kuondokana na adha ya kupata leseni.

Nae, Mwenyekiti wa shirikisho hilo, Said Chenje amemuhakikishia DC huyo watafanya kazi kwa ukaribu na Jiji la Dar es  Salaam na Jeshi la Poisi Usalama Barabarani ili madereva Bodaboda waweze kufauata kutii sheria hizo. 


No comments:

Post a Comment

Pages