HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 01, 2023

Mzumbe yawakaribisha wananchi kutembelea banda lao Sabasaba


 
Afisa Udahili Chuo Kikuu Mzumbe, Nringi  Urassa, akitoa maelezo kwa wanafunzi waliotembelea banda la Chuo hicho kwenye Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) Julai 1, 2023.
Kaimu Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaalam( DVC ARC) Dkt. Eliza Mwakasangula(kulia) akiangalia Moja wapo ya bidhaa zilizotengenezwa na Mercy Mwambe , Mwanafunzi wa Masomo ya Shahada ya Uongozi wa Biashara katika Ujasiliamali na Ubunifu (BBA EIM).
Mhitimu wa Chuo Kikuu Mzumbe 2022, Aron Msonga, akichangia fedha kwa ajili ya
Ujenzi Hosteli ya Wanafunzi wa Kike Ndaki ya Mbeya, alipotembelea Banda la Chuo hicho kwenye Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Kimataifaji na Baraza la Wahitimu Chuo Kikuu Mzumbe, Dk. Lucy Massoi.
Mkurugenzi wa Kimataifaji na Baraza la Wahitimu Chuo Kikuu Mzumbe, Dk. Lucy Massoi (kushoto) akionesha muhamala aliochangia mhitimu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Martine Thomas, kwa ajili ya Ujenzi Hosteli ya Wanafunzi wa Kike Ndaki ya Mbeya, alipotembelea Banda la Chuo hicho kwenye Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) jijini Dar es Salaam.




 

Na Tatu Mohamed, Dar es Salaam


KAIMU Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe  anaeshughulikia taaluma, utafiti na ushauri, Dk. Eliza Mwakasangula amewakaribisha Watanzania wote kutembelea banda lao lililopo katika Maonesho ya Biashara ya 47 ya Kimataifa (Sabasaba) yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.

Akizungumzia katika viwanja hivyo amesema katika huduma mbalimbali ambazo zinatolewa katika chuo hicho hivyo wafike kuweza kujionea.

"Tunawakaribisha watu wote kwani tunahuduma mbalimbali, tunadahili wanafunzi kwaajili ya kujiunga na Program zetu Chuo Kikuu Mzumbe kwa ngazi ya Shahada za awali kwa wale waliomaliza kidato cha nne, kidato cha Sita na hata waliomaliza muda mrefu," amesema.

Amesema Chuo Kikuu cha Mzumbe ni miongoni mwa vyuo vinavyotoa Mafunzo mbalimbali ikiwemo masomo ya Biashara, Utawala, Sheria, Uhasibu, Sayansi na Teknolojia ambapo wanateknolojia mbalimbali kwa vijana wao ambao wamekuwa wakizianzisha chuoni hapo.

"Chuo chetu kina kampasi tatu ambapo ni  Mkoa wa Morogoro, Dar es Salaam maeneo ya Upanga na Tegeta pamoja na mkoani Mbeya," amesema.

Aidha Dk. Eliza amewaomba Watanzania wakiwemo Wanafunzi waliomaliza Chuo hicho miaka ya nyuma (Alumni) kujitokeza na kuchangia kampeni ya ujenzi wa bweni la wanafunzi wa kike mkoani Mbeya.

Amesema kwa kufanya hivyo ni ishara ya 
kurudisha kitu kidogo kwa jamii ikiwa nao ni wanajamii wa Chuo Kikuu Mzumbe.

"Ujenzi wa bweni hilo tayari umezinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ambapo  kuna namba maalum ya uchangiaji hivyo  niwakaribishe wanafunzi waliosoma Mzumbe kuweza kuchangia," amesema.

Licha ya kuwakaribisha pia amewaomba wananchi kwa ujumla kuchangia ujenzi wa hosteli za Wanachuo wa kike katika kampasi ya Mbeya kupitia control namba 994180331310.


No comments:

Post a Comment

Pages