Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania, Prof. Charles Kihampa, akizungumza na waandishi wa habari wakati akitangaza kufunguliwa kwa dirisha la udahili kwa waombaji wa Shahada ya Kwanza kuanzia kwa mwaka wa masomo 2023
Na Mwandishi Wetu
TUME
ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imefungua dirisha la maombi ya udahili kwa
waombaji wa shahada ya kwanza wa mwaka wa masomo 2023/2024 kuanzia leo
Julai 15, 2023 huku ikianisha sifa zinazohitajika kwa wanafunzi kusoma
katika vyuo vikuu mbali mbali nchini.
Katibu
Mtendaji wa TCU, Prof.Charles Kihampa amesema dirisha litakuwa wazi
hadi Agosti 4, 2023 na kuwahimiza waombaji wote wa udahili kuendelea
kupata taarifa sahihi kupitia tovuti ya TCU au tovuti za Vyuo mbalimbli
vinavyotoa elimu ya juu.
Waombaji
wote wa udahili kwa mwaka wa masomo 2023/2024 wanatakiwa kuwa na sifa
stahiki za kidato cha sita, sifa stahiki za Stashahada na Cheti cha
awali.
"Maombi ya udahili
wa kujiunga na Shahadawa kujiunga na shahada ya kwanza utahusu waombaji
waliohitimu wa kidato cha sita, wenye Stashahada (Ordinary Diploma), na
wenye sifa swahili za cheti cha awali (Foundation Certificate) ya
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT).
Ili
kufahamu sifa stahiki za kujiunga na Chuo Kikuu waombaji wameelekezwa
kusoma vigezo vilivyopo kwenye vitabu vya muongozo vya TCU huku pia
wakitakiwa kutuma maombi yao moja kwa moja kwenye vyuo ambavyo
wamevichagua na kwamba maelekezo ya jinsi ya kutuma maombi yanayotolewa
na vyuo vikuu husika.
Aidha
Prof. Kihampa amewapa tahadhari waombaji wote wa shahada ya kwanza
ikiwa watahitaji kupata ufafanuzi wa suala lolote juu ya udahili
kuwasiliana moja kwa moja na vyuo husika ama TCU.
"Tunawaasa
wananchi kuepuka kupotoshwa na watu wanaojiita mawakala au washauri
wanaodai wanatoa huduma ya jinsi ya kujiunga na vyuo vya elimu ya juu
hapa nchini" amesema Prof. Kihampa.
Amesema
masuala muhimu ambayo waombaji wanapaswa kuzingatia ni pamoja na kusoma
muongozo wa udahili na kuuelewa, kuingia kwenye tovuti za vyuo ili
kujua taratibu za kutuma maombi, kutuma maombi moja kwa moja vyuoni
kupitia mifumo ya kielektoniki na kuwasiliana na vyuo ili kupata taarifa
huku pia waombaji wenye vyeti vinavyoytolewa na NECTA au NACTE
wakitakiwa kupata idhibati ya ulinganifu wa sifa zao kabla ya kutuma
maombi ya udahili.
Aidha
Tume inawakaribisha wadau wote kushiriki maonesho ya 18 ya Elimu ya Juu,
Sayansi na Teknolojia yatakayofanyika viwanja vya Mnazi Mmoja, Jijini
Dar es Salaam kuanzia Jula 17 hadi 22 mwaka huu ambapo vyuo 80
vinatarajiwa kuwepo katika maonesho hayo.
No comments:
Post a Comment