HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 01, 2023

MIZENGO PINDA AFUNGUA MAFUNZO YA VIONGOZI SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU NYERERE


 Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda akizungumza kwenye ufunguzi wamafunzo ya Uongozi  kwa viongozi  leo Julai 31  kwenye Shule  ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere iliyopo  maeneo ya ya Kwamfipa wilayani Kibaha mkoani Pwani.

 

Na Khadija Kalili

WAZIRI Mkuu Mstaafu wa awamu ya tatu  Mheshimiwa Mizengo Kayanza  Peter  Pinda  leo amefungua mafunzo kwa Viongozi  kutoka katika Taasisi mbalimbali  za seeikali  mafunzo hayo ya Uongozi na Maadili yanayofanyika kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere iliyopo Wilayani Kibaha Mkoani Pwani.

Akifungua mafunzo hayo leo Julai 31  wa  Chama na Serikali  kujiendeleza  na elimu ya Uongozi ili waweze kuwasimamia vyema wanaowaongoza  katika sehemu zao za  kazi  huku amesema kuwa    kwamba elimu haina mwisho.


Amesema kuwa upo umuhimu wa  akitoa wito wa kuwaendeleza wataalamu  mbalimbali  kwa lengo la kuwajengea uwezo ,uzalendo wa nchi yao jambo ambalo litachochea wqtu kufanya kazi kwa bidii, juhudi,maarifa makubwa na kutojali kuona wanapoteza nguvu zao kwa kiasi gani.

 "Uzalendo ni dhana yenye wigo mpana zaidi hivyo jambo hili ni la muhimu mtu kukaa darasani na kupikwa ili pindi anapomaliza mafunzo haya atoka akiwa  ameiva  na kuelewa dhana halisi ya kua mzalendo ndani ya nchi yako, zamani viongozi  walipikwa pindi walipoteuliwa tofauti na ilivyo sasa hivyo ili  kuongeza ufanisi katika uongozi  nashauri viongozi wakiwemo Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na watu wa kada mbalimbali  wawekewe utaratibu  wa kupata mafunzo kama haya mara kwa mara"amesema Mheshimiwa  Pinda.

Akifungua mafunzo hayo ya wiki moja Mheshimiwa  Pinda amesema kuwa amefurahishwa kuona uwiano wa washiriki wa mafunzo hayo ambapo jinsia zote zimeshirikiswa ipasavyo.

Amesema kuwa wakati umefika wa  kuwajengea uzalendo wananchi wa kada zote wakiwamo wanafunzi  huku akitolea mfano wa nchi ya Izrael namna ambavyo wamewajengea  wananchi wao kuipenda na kuithamini nchi yao huku akisema kuwa kila Mtanzania  anapaswa kuwa mzalendo licha ya kuwa na itikadi tofauti za kidini, kabila  na rangi lakini wote wawe  kitu kimoja.

Ametoa sifa kwa uongozi  wa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere  kuwa licha ya kuwa hakina muda mrefu lakini matunda yake yameanza kuonekana na maua yake yamechanua kutokana na mafunzo waliyopatiwa watu  mbalimbali wakiwemo wanasiasa , viongozi wa  ndani na nje ya nchi.

"Viongozi  wangu katika serikali naomba tuwajibike kikamilifu, kwanza wajibika halafu dai haki yako  kila Kiongozi  anapaswa kuwa mbunifu na mzalendo katika Taasisi yake na  kuwajibika ipasavyo.

"Mashirika makubwa na Taasisi nyingi za serikali  zinayumba sababu Viongozi  wengi siyo waadilifu,kitu kinachoitwa uadilifu ni kigumu lakini endapo utakaa na kina babu ambao ni wakongwe  kuna mambo  mazuri  unaweza kuyapata  binafsi naweza sema nimepata bahati ya kufanya kazi  na viongozi   wakongwe  wengi ambao ndiyo walionijenga  natumia mfano huu ikiwa ni lengo la kutaka kuwakumbusha  umuhimu wa kuthamini wazee katika utendaji  wetu" amesema Pinda.

"Nasisitiza uadilifu na kuacha maovu ambayo yanaathiri jamii kwa ujumla ndiyo maana CAG akitoa ripoti  yake inakua imejaa madudu mengi yote haya ni  kutokana na upungufu wa maadili  ya uongozi kwa baadhi ya viongozi  nchini ". amesema  Waziri Mkuu Mstaafu wa awamu ya tatu Mheshimiwa  Pinda.

Ametoa rai  kwa uongozi  wa Shule ya Mwalimu Nyerere kuwepo na utaratibu wa kutoa mafunzo  mafupi yanayohusu uongozi, uzalendo  na  uendeshaji nchi kwa ujumla .

"Wateule  wote wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) jipangeni ili mje kupata mafunzo hapa itumieni  fursa ya Shule hii ya siasa kuwapika makada wa chama ili waweze kukinadi chama kwa weledi wa hali ya juu"amesema.

Mkuu wa Shule hiyo ya Mwalimu Nyerere Prof.Marceline Chijoliga  amesema kuwa  wanajivunia kwa kutoa mafunzo bora  kwani hadi sasa  tayari zaidi ya wahitimu 2,000 wamepata mafunzo katika  Shule hiyo.

"Mapema mwezi huu jumla ya viongozi  wanawake 71 wamehitimu mafunzo  yaliyowashirikisha  washiriki kutoka katika Taasisi mbalimbali  nchini  na wamehitimu vyema hivyo tunatarajia watakua viongozi bora huko waliko,  mafunzo waliyopata  yamewajengea uwezo viongozi hao wanawake  na ambao wanauzoefu  siyo chini ya miaka mitano ambayo yamefanyika kwa mara yakwanza hapa nchini  ambapo wahitimu wamefundishwa  mbinu bora  za Uongozi  wa Utawala  Bora  katika Taasisi wanazoziongoza.


Aidha ufunguzi huo umehudhuriwa na viongozi wa chama na serikali akiwamo Mheshimiwa  Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson Simon , Mwanasiasa Mkongwe  nchini  ambaye ameshika nyadhifa mbalimbali  Mzee Paul Kimiti.

Mstaafu Paul Kimiti amewahimiza  viongozi hao kuwa wazalendo ndani ya nchi yao.

Amesema kuwa hakuna aliye  juu zaidi ya mwingine hivyo amesisitiza kuwa kila mmoja anamtegemea mwenzake  na kusema kuwa katika maisha epuka  kufanya  maamuzi katika jambo lolote  bila kushirikisha  wenzako wengine wanao kuzunguka kwani  hiyo  ndiyo sifa ya Kiongozi  bora.

"Kiongozi bora huheshimu   anaowaongoza na kuwashirikisha   bila ya kujali umri ,itikadi zao za  dini na mambo mengineyo yanayowatofautisha.
 

No comments:

Post a Comment

Pages